Zaburi 4:1-8

  • Sala ya kumutegemea Mungu

    • “Mukasirike, lakini musitende zambi” (4)

    • ‘Nitalala usingizi kwa amani’ (8)

Kwa kiongozi; iimbwe kwa vyombo vya kamba. Muziki wa Daudi. 4  Wakati ninakuita, unijibu, Ee Mungu wangu mwenye haki.+ Unitengenezee njia ya kuponyoka* taabu yangu. Unionyeshe wema na usikie sala yangu.   Ninyi wana wa binadamu, mutaendelea mupaka wakati gani kugeuza heshima yangu kuwa haya? Mutaendelea mupaka wakati gani kupenda mambo yenye hayana mafaa yoyote na kutafuta mambo ya uongo? (Sela)   Mujue kwamba Yehova atamutendea mushikamanifu wake kwa njia ya pekee;* Yehova atasikia wakati nitamuita.   Mukasirike, lakini musitende zambi.+ Museme katika moyo wenu, kwenye kitanda chenu, na munyamaze kimya. (Sela)   Mutoe zabihu za haki, Na mumutegemee Yehova.+   Kuko watu wengi wenye kusema: “Ni nani atatuonyesha jambo lolote la muzuri?” Mwangaza wa uso wako utuangazie, Ee Yehova.+   Umejaza moyo wangu shangwe nyingi sana Kuliko wale wenye kuwa na mavuno mengi sana ya nafaka na divai mupya.   Nitajilaza chini na kulala usingizi kwa amani,+ Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, unanifanya niishi katika usalama.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Unitengenezee nafasi kubwa katika.”
Ao “atamufanya mushikamanifu wake aonekane kuwa tofauti; atamutia pembeni mushikamanifu wake kwa ajili yake mwenyewe.”