Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kusamehe kunaweza kuzimisha moto wa kukosa kuelewana

KWA AJILI YA BIBI NA BWANA

4: Kusameheana

4: Kusameheana

MAANA YAKE NINI?

Kusamehe kunamaanisha kuachilia kosa na kuepuka kinyongo chenye kinaweza kutokezwa na kosa hilo. Kusamehe hakumaanishe kwamba unapaswa kupunguza uzito wa kosa ao kufanya kama vile kosa halikufanyika hata kidogo.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari [ao, kwa kupenda] ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.’​—Wakolosai 3:13.

“Ikiwa unapenda mutu, hautakazia uzaifu wake, lakini utaona sifa za muzuri zenye mutu huyo anajikaza kuonyesha.”​—Aaron.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Ikiwa unaweka kinyongo, unaweza kujilitea wewe mwenyewe matokeo ya mubaya juu ya afya yako ya kimwili na ya kiakili; unaweza pia kuharibu ndoa yenu.

“Siku moja bwana yangu aliniomba musamaha juu ya jambo fulani lenye liliniumiza sana. Ilikuwa nguvu kwangu kumusamehe. Nilifikia kumusamehe, lakini ninahuzunika juu ya nini sikufanya hivyo haraka. Hilo lilileta mahangaiko yenye haiko ya lazima katika ndoa yetu.”​—Julia.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

UJICHUNGUZE

Wakati mwingine wenye bibi ao bwana yako anasema ao kufanya jambo fulani lenye linakuumiza, ujiulize:

  • ‘Ninakasirika haraka?’

  • ‘Kosa ni kubwa sana hivi kwamba ni lazima mwenzangu aniombe musamaha, ao ni jambo lenye ninaweza tu kusahau?’

ZUNGUMUZA NA BIBI AO BWANA YAKO

  • Kwa kawaida, inatuomba muda gani ili tufikie kusameheana?

  • Tunaweza kufanya nini ili tufikie kusameheana bila kukawia?

MASHAURI

  • Wakati bibi ao bwana yako anakukosea, usifikiri kuwa amechochewa na nia ya mubaya.

  • Ujikaze kusamehe matendo ya bibi ao bwana yako, ukikumbuka kuwa ‘sisi wote tunajikwaa mara nyingi.’​—Yakobo 3:2.

“Ni mwepesi kusamehe wakati sisi wote tuko na kosa, lakini ni nguvu zaidi wakati inaonekana kuwa ni mutu mumoja tu ndiye amefanya kosa. Kukubali wakati mutu anaomba musamaha na kumusamehe inaomba unyenyekevu wa kweli.”​—Kimberly.

KANUNI YA BIBLIA: “Ukuwe tayari kusuluhisha [ao, kumaliza] mambo upesi.”​—Mathayo 5:25.

Ikiwa unaweka kinyongo, unaweza kujilitea wewe mwenyewe matokeo ya mubaya juu ya afya yako ya kimwili na ya kiakili; unaweza pia kuharibu ndoa yenu