Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Ufundi wa Kusafiri wa Kidudu Mbawakawa

Ufundi wa Kusafiri wa Kidudu Mbawakawa

MBAWAKAWA anatumia mavi kwa njia nyingi. Anakula mavi, anataga mayai juu yake. Mbawakawa fulani wa kiume anamupatia mbawakawa wa kike kipande kikubwa cha mavi ili kumutongoza. Mbawakawa wanagombania sana mavi yenye kuwa teketeke. Wakati fulani wachunguzi waliona mbawakawa karibu 16000 wakizunguka kwa uwingi mavi ya tembo, na kuyaondoa kwa muda wa saa mbili tu.

Aina fulani za mbawakawa ambao wanakula mavi wanajitenga na wadudu wengine kwa kukata sehemu ya mavi na kuifanya kuwa na umbo la muviringo, wanayapeleka mbali kwa kuyazungusha-zungusha, na kisha wanayazika ndani ya udongo wa teketeke. Mbawakawa anapeleka mavi ambayo alichukua kwa kufuata njia iliyonyoroka, kwa sababu kufanya hivyo kunamusaidia aendelee mbele haraka na kunasaidia mavi anayochukua yasikamatwe na vidudu wengine.

Lakini ni nini kinamusaidia kidudu mbawakawa kwenda kwa kufuata njia iliyonyoroka, zaidi sana usiku?

Fikiria hili: Uchunguzi uliofanywa hapo mbele umeonyesha kwamba mbawakawa wanaweza kusafiri kwa kufuata mwangaza wa jua ao wa mbalamwezi, lakini wanaweza pia kusafiri kwa kufuata njia iliyonyoroka hata ikiwa ni usiku wenye giza kidogo. Wachunguzi katika inchi ya Afrika ya Kusini walivumbua kwamba mbawakawa wanafanya hivi, si kwa kuona nyota moja moja, lakini wanafuata muangaza unaotoka kwenye nyota za galaksi yetu. Kulingana na gazeti moja, vidudu hivyo “ndivyo vitabu vinataja kwa mara ya kwanza kwamba vinasaidiwa na mwangaza wa galaksi yetu ili kusafiri.” (Current Biology)

Muchunguzi mumoja, Marcus Byrne, anasema kwamba mbawakawa wana “uwezo muzuri wa kuona wakati wanasafiri. Uwezo huo unawasaidia hata wakati kuna mwangaza muchache sana wa nyota, wakitumia uwezo mudogo wa akili yao.” Anaongeza kusema hivi: “Wanaweza kuwafundisha watu namna ya kumaliza matatizo makubwa ya kuona.” Kwa mufano, mashini inayoitwa roboti inaweza kutengenezwa ili kuchunguza nyumba ambayo imeanguka kwa kuiga ufundi wa kusafiri wa mbawakawa.

Unawaza namna gani? Je, uwezo wa mbawakawa ambaye anakula mavi ulijitokeza wenyewe? Ao kuna muumbaji aliyemupatia uwezo huo?

Je, ulijua?

Mbawakawa wanalisha udongo na kuufanya uwe teketeke, wanatawanya mbeguza mimea, na wanazuia inzi.