Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Kifo

Kifo

Watu waliokufa wako wapi?

‘Wewe ni mavumbi nawe utarudi katika mavumbi.’—Mwanzo 3:19.

MAWAZO YA WATU

Watu fulani wanafikiri kwamba kisha kifo watu wanaendelea kuishi mbinguni, katika moto wa mateso, katika pirgatori ao Limbo (mahali ambapo roho za watoto na watu wazuri wasiobatizwa zinaenda). Watu wengine wanaamini kwamba mutu anazaliwa tena katika mwili mwingine. Kwa upande mwengine, wale wanaokataa mafundisho ya dini wanaamini tu kwamba kifo ni mwisho wa maisha ya mutu.

MAWAZO YA BIBLIA

Andiko la Mhubiri 9:10 linasema kwamba “hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.” Biblia inaeleza pia namna watu na wanyama wanakuwa wakati wanakufa. Inasema hivi: ‘Wote wanaenda mahali pamoja. Wote wametoka katika mavumbi, nao wote wanarudi katika mavumbi.’—Mhubiri 3:20.

Watu waliokufa wako katika hali gani?

‘Roho yake inatoka, naye anarudi kwenye udongo wake; siku hiyo mawazo yake yanapotea.’—Zaburi 146:4.

MAWAZO YA WATU

Watu wengi wamefundishwa kwamba hali ya mutu kisha kifo inategemea mambo ambayo alifanya wakati alikuwa angali muzima katika dunia. Ikiwa alifanya mema, atapata furaha ya milele; ikiwa alifanya mabaya, atateswa milele. Wengi wanafikiri kwamba watu wanapaswa kusafishwa ili kuondoa zambi ndani yao mbele ya kuruhusiwa kuenda mbele ya Mungu kisha kifo. Wale ambao hawasafishwe hawawezi kupata pendeleo hilo milele.

MAWAZO YA BIBLIA

Watu waliokufa hawako katika furaha ao katika mateso. Kwa sababu hawajue kitu, hawawezi kupatwa na jambo lolote, hawawezi kusaidia ao kuumiza watu walio wazima. Andiko la Mhubiri 9:5,6 linaonyesha kwamba ‘walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajue lolote kamwe, ... Pia, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, na mupaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua.’

Kuna tumaini kwa watu waliokufa?

‘Mutu akikufa, anaweza kuishi tena? Mimi nitangojea siku zote za kazi yangu ya kulazimishwa, mupaka kitulizo changu kikuje.’—Ayubu14:14.

MAWAZO YA WATU

Watu wengi wanaamini kwamba wakati mutu anatupwa katika moto wa mateso, hakuna tena tumaini kama anaweza kuishi tena. Wanasema kwamba mutu anateseka humo milele. Kwa upande mwengine, inasemekana kama wale walio katika pirgatori wanaenda katika furaha ya milele kisha wao kusafishwa kwa moto ili zambi zao ziondolewe.

MAWAZO YA BIBLIA

Kisha kupumuzika katika kifo, watu ambao wamekufa watafufuliwa na Mwana wa Mungu ili waishi katika dunia. Biblia inasema hivi: ‘[Musishangae juu ya] jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote walio ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka.’ (Yohana 5:​26, 28, 29) Mambo ambayo mutu atafanya kisha kufufuliwa yataonyesha ikiwa atapata uzima wa milele ao hapana. *

^ fu. 14 Ili kupata habari zingine juu ya ufufuo, tafazali soma sura ya 7 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.