Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI FULANI ZA ULIMWENGU

Habari Fulani za Afrika

Habari Fulani za Afrika

Mashirika mengi na watu wengi wanaendelea kujikaza ili kufanya maisha katika Afrika yakuwe muzuri zaidi. Lakini, sehemu hii ya dunia ingali na matatizo makubwa sana.

KUWINDA VIFARU KINYUME NA SHERIA

Katika mwaka wa 2013, vifaru (rhinocéros) 1 004 waliuawa kinyume na sheria katika inchi ya Afrika Kusini. Katika mwaka wa 2007, ni vifaru 13 tu ndio waliuawa. Hata kama hesabu hiyo kubwa inatolewa, pembe za vifaru zinaendelea kutafutwa sana; kilogramu moja ya pembe hizo iko na bei kupita kilogramu moja ya zahabu. Bei ya pembe moja ya kifaru inaweza kufikia dola elfu mia tano.

Fikiria jambo hili: Kuna siku serikali zitaweza kumaliza uvunjaji wa sheria?—Yeremia 10:23.

RUSHWA ISIYOJULISHWA

Shirika linalochunguza mambo ya rushwa (Transparency International) linasema kuwa inchi za Mashariki mwa Afrika ziko kati ya inchi zenye kuwa na rushwa (kata-midomo, hongo) sana katika dunia. Lakini, watu 90 juu ya 100 wenye wanakutana na rushwa hawajulishe serikali. Musemaji mumoja wa shirika hilo katika inchi ya Kenya anasema hivi: “Inaonekana kuwa raia hawatumaini kama serikali zitafanya jambo fulani kisha kujulishwa juu ya rushwa.”

Mambo Biblia Inasema: ‘Rushwa inapofusha watu wanaoona vizuri.’​—Kutoka 23:8.

Habari fulani za Afrika

Kulingana na shirika la mawasiliano la Umoja wa Mataifa, ilitazamiwa kuwa kufikia mwisho wa mwaka wa 2014, Waafrika karibu 20 juu 100 watakuwa wanatumia Internete. Hesabu ya watu wenye wanajiandikisha kwenye Internete kupitia vyombo vyao vya mukononi inaongezeka mara mbili kuliko hesabu ya watu wote wenye wanafanya hivyo katika dunia yote.