Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Kushugulika na Wazazi Wakwe

Kushugulika na Wazazi Wakwe

TATIZO

“Wakati tulikuwa na magumu, bibi yangu aliambia wazazi wake juu ya magumu yetu. Kisha baba yake aliniita ili kunipatia mashauri juu ya hali hiyo. Sikufurahia kabisa jambo hilo!”—James. *

“Mara nyingi mama yangu mukwe anasema hivi: ‘Ninakumbuka kijana wangu sana!’ Anaeleza namna walikuwa wanapendana sana, na hilo linafanya nijisikie kuwa nilifanya makosa kuolewa naye na kufanya mama yake aumie moyoni!”—Natasha.

Inawezekana kufanya tatizo pamoja na wazazi wakwe lisilete shida katika ndoa?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Ndoa inaanzisha familia mupya. Biblia inasema kuwa mwanaume mwenye anaoa ‘atamuacha baba yake na mama yake naye atashikamana na muke [bibi] wake.’ Mwanamuke pia anaacha wazazi wake na kushikamana na bwana yake. Wakati anaolewa, Biblia inasema kuwa wote wawili wanakuwa ‘mwili mumoja.’ Wanaanzisha familia mupya.—Mathayo 19:5.

Munapaswa kutanguliza ndoa yenu kuliko wazazi wenu. John Gottman, mushauri wa mambo ya ndoa, aliandika hivi: “Kati ya mambo ya maana sana yenye ndoa inatimiza, jambo moja ni kufanya bibi na bwana ‘wafikiriane.’ Ili kufanya ao kurudisha umoja kati yako na bibi ao bwana yako, inaweza kuomba pia kuachana na familia yako ya mbele kwa kadiri fulani.” *

Inaweza kuwa vigumu kwa wazazi fulani kuzoea hali ya mupya. Mwanaume mumoja kijana anasema hivi: “Mbele nioe bibi yangu, kila mara alikuwa anatanguliza mambo wazazi wake wanapenda. Kisha ndoa yetu, mama yake aliona kuwa mutu mwengine alikamata nafasi ya kwanza. Haikukuwa vyepesi kwake kukubali jambo hilo.”

Inaweza kuwa vigumu pia kwa bibi na bwana fulani wapya katika ndoa. James, mwenye tumekwisha kutaja, anasema hivi: “Kuwa na wazazi wakwe haiko kama kuwa na marafiki wenye ulijichagulia. Ni kama vile mutu anakuambia, ‘Uko na marafiki wapya wawili upende usipende.’ Hata kama wanakukasirisha, ni watu wa familia yako!”

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Ikiwa wewe na bibi ao bwana yako hamukubaliane juu ya hali fulani kuhusu wazazi wakwe, mujikaze kumaliza magumu hayo katika roho ya umoja. Fuata shauri hili la Biblia: “Utafute amani, na kuifuatia.”—Zaburi 34:14.

Ili kukusaidia kufanya hivyo, fikiria hali zenye kufuata. Katika kila hali, ni bibi ao bwana ndiye mwenye kuwa na tatizo. Lakini, matatizo yenye kuonyeshwa katika hali zote yanahusu wote wawili, na kanuni zenye zinazungumuziwa zinaweza kuwasaidia kumaliza matatizo mengi yenye kuhusu wazazi wakwe.

Bibi yako anasema kuwa angependa ukuwe na uhusiano muzuri na mama yake. Lakini unamuona mama yake kuwa mutu mugumu.

Jaribu kufanya hivi: Zungumuza na bibi yako juu ya tatizo hilo, na ukuwe tayari kukubali mawazo yake. Jambo la maana haiko namna unaona mama yako mukwe, lakini namna unaona bibi yako, mwenye uliapa kupenda. Katika mazungumuzo hayo, tafuta jambo moja ao mambo mawili yenye unaweza kufanya ili kuwa na uhusiano muzuri zaidi na mama yake, na uyatimize. Wakati bibi yako ataona namna unajikaza kufanya hivyo, atakuheshimia zaidi.—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 10:24.

Bwana yako anasema kama unafurahia sana kupendeza wazazi wako kuliko kumupendeza yeye.

Jaribu kufanya hivi: Zungumuza na bwana yako juu tatizo hilo, na ujaribu kujitia pa nafasi yake. Kwa kweli, bwana yako hapaswe kuhuzunika kwa sababu tu unawapatia wazazi wako heshima yenye wanastahili. (Methali 23:22) Lakini, inaweza kuwa lazima umuhakikishie, kupitia maneno na matendo yako, kama ni yeye unatanguliza katika maisha yako lakini haiko wazazi wako. Kama bwana yako anakuwa na uhakika huo, pengine hatajisikia kuwa unafurahia kupendeza wazazi wako kumupita.—Kanuni ya Biblia: Waefeso 5:33.

Bibi yako anawaomba wazazi wake mashauri kuliko kukuomba wewe.

Jaribu kufanya hivi: Zungumuza na bibi yako, na mukubaliane juu ya mipaka yenye munapaswa kujitilia. Usiweke mipaka yenye kupita kiasi. Ni mubaya kila mara kuzungumuza na muzazi juu ya tatizo fulani? Ni wakati gani inaweza kufaa kufanya hivyo? Ikiwa munakubaliana juu ya mipaka yenye kufaa, jambo hilo halitakuwa tatizo.—Kanuni ya Biblia: Wafilipi 4:5.

[Maelezo ya chini]

^ fu. 4 Majina yamebadilishwa katika habari hii.

^ fu. 9 Kutoka katika kitabu The Seven Principles for Making Marriage Work.