Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | KUSALI KUNALETA FAIDA FULANI?

Sababu Gani Mungu Anatuomba Tusali?

Sababu Gani Mungu Anatuomba Tusali?

Mungu anapenda tukuwe marafiki wake.

Marafiki wanazungumuza ili wakuwe na urafiki muzuri zaidi. Mungu pia anatuomba tuzungumuze naye, kwa kufanya hivyo anatupatia nafasi ya kuwa na urafiki muzuri pamoja naye. Anasema hivi: ‘Mutaniita na kuja na kusali kwangu, nami nitawasikiliza.’ (Yeremia 29:12) Kuzungumuza na Mungu kupitia sala kutatusaidia ‘kumukaribia Mungu, naye atatukaribia.’ (Yakobo 4:8) Biblia inatuhakikishia hivi: ‘Yehova iko karibu na wote wanaomuitia.’ (Zaburi 145:18) Kama tunazoea kusali, urafiki wetu pamoja na Mungu utakomaa.

‘Yehova iko karibu na wote wanaomuitia.’—Zaburi 145:18

Mungu anapenda kukusaidia.

Yesu alisema hivi: ‘Ni nani kati yenu ambaye mwana wake akimuomba mukate—je, atamupa jiwe? Kwa hiyo, ikiwa ninyi . . . munajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo nzuri, je, Baba yenu aliye mbinguni hatawapa hata zaidi vitu vyema wale wanaomuomba?’ (Mathayo 7:9-11) Ndiyo, Mungu anakuomba usali kwa sababu “yeye anakujali [anakuhangaikia]” na anataka kukusaidia. (1 Petro 5:7) Anakuomba hata umuelezee magumu yako. Biblia inatuambia hivi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote, bali [lakini] katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.’—Wafilipi 4:6.

Wanadamu wako na uhitaji wa kiroho.

Watu wenye elimu ya hali ya wanadamu wametambua kama mamilioni ya watu wanaona ulazima wa kusali. Hata watu fulani wenye kuamini kama hakuna Mungu na wenye kuamini kama mambo yake hayawezi kujulikana, wako na ulazima huo. * Jambo hilo linahakikisha kama wanadamu waliumbwa na ulazima wa kiroho. Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji [ulazima] wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3) Njia moja ya kutimiza ulazima huo ni kuzungumuza kwa ukawaida na Mungu katika sala.

Ikiwa tunasali kama vile Mungu anatuomba, tutapata faida gani?

^ fu. 8 Uchunguzi wenye ulifanywa na Kituo cha Utafiti cha Pew katika mwaka wa 2012, ulionyesha kama katika inchi ya Amerika, watu 11 juu 100 wenye kuamini kama hakuna Mungu na wenye kuamini kama mambo yake hayawezi kujulikana, wanasali mara moja hivi katika mwezi.