Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Sasa Ninajisikia Kuwa Ninaweza Kusaidia Wengine

Sasa Ninajisikia Kuwa Ninaweza Kusaidia Wengine
  • ALIZALIWA MWAKA WA : 1981

  • INCHI : GUATEMALA

  • ALIKUWA: NA HALI NGUMU WAKATI ALIKUWA MUTOTO

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

Nilizaliwa Acul, muji wa mbali sana katika maeneo ya milima upande wa mangaribi mwa Guatemala. Familia yetu ni ya kabila la Ixil, kabila hilo lilitokana na Wamaya. Zaidi ya luga ya Kihispania, nilikuwa ninazungumuza pia luga yetu ya kienyeji wakati nilikuwa ninakomaa. Katika miaka yangu ya kwanza ya maisha, kulikuwa kipindi kigumu katika inchi ya Guatemala, ni kusema, vita ya watu wenyewe kwa wenyewe yenye ilifanya miaka 36. Katika kipindi hicho, watu wengi wa kabila la Ixil walikufa.

Wakati nilikuwa na miaka ine, ndugu yangu mukubwa mwenye miaka saba alikuwa anacheza na grenade, kisha ikalipuka bila kutazamia. Kwa sababu ya aksidenti hiyo, nikakuwa kipofu na jambo la kuhuzunisha ni kwamba ndugu yangu huyo alikufa. Kwa hiyo, nilipitisha maisha yangu ya utoto kwenye masomo ya vipofu katika muji wa Guatemala City, kwenye nilijifunza kusoma Maandishi ya Vipofu. Na kwa sababu zenye sikuelewa muzuri, walimu walinikataza kuzungumuza na watoto wengine na wanafunzi wenzangu walikuwa wananiepuka. Sikuzote nilikuwa peke yangu na nilikuwa ninangojea kwa hamu miezi mbili kila mwaka wakati ningeweza kuenda nyumbani ili kuwa na mama yangu, ambaye sikuzote alikuwa mutu muzuri na mwenye huruma. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, alikufa wakati nilikuwa na miaka kumi. Nilijisikia kuwa nimepoteza mutu mumoja tu mwenye alinipenda katika dunia yote, nilivunjika moyo sana.

Wakati nilikuwa na miaka 11, nilirudia katika muji wetu na nikaanza kuishi katika familia ya ndugu yangu mwenye tulizaliwa naye baba mumoja lakini mama tofauti. Walinipatia mambo ya kimwili yenye nilikuwa nayo lazima, lakini hakuna mutu aliweza kunisaidia katika hali yangu ya moyoni. Wakati fulani, nilikuwa ninamulilia Mungu hivi: “Sababu gani mama yangu alikufa? Sababu gani niko kipofu?” Watu walikuwa wananiambia kama taabu hizo zilikuwa mapenzi ya Mungu. Niliona kuwa Mungu hana moyo wa huruma na hatende kwa haki. Sababu moja tu yenye ilifanya nisijiue ni kukosa njia ya kufanya hivyo.

Kuwa kipofu kulifanya nikuwe muzaifu katika hali ya kimwili na ya moyoni. Wakati nilikuwa kijana mudogo, mara nyingi nililalwa kinguvu. Sikuambia mutu yeyote matendo hayo mabaya, kwa sababu niliona kama hakuna mutu angenihangaikia. Watu hawakuzoea kuzungumuza na mimi, na sikuzungumuza na mutu yeyote. Nilijitenga na watu, nilikuwa mwenye huzuni nyingi, na sikutumainia mutu yeyote.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

Wakati nilikuwa na miaka 13, Mashahidi wawili wa Yehova (bibi na bwana) walikuja kuniona wakati wa mapumziko kwenye masomo. Mumoja kati ya walimu wangu wa masomo, mwenye alihangaikia hali yangu, alikuwa amewaomba wakuje kuniona. Mashahidi hao walizungumuza na mimi juu ya ahadi ya Biblia yenye kuonyesha kama wafu watafufuliwa na kama siku moja vipofu wataona tena. (Isaya 35:5; Yohana 5:28, 29) Nilifurahia mambo yenye walinifundisha, lakini ilikuwa vigumu kuzungumuza nao, kwa sababu sikuzoea kuzungumuza na watu. Lakini, hata kama sikukuwa ninazungumuza sana, walinionyesha upole na uvumilivu, waliendelea kunitembelea ili kunifundisha Biblia. Mashahidi hao walikuwa wanatembea kilometa zaidi ya 10 na kwenye milima ili kufika katika muji wetu .

Ndugu yangu alinifasiria kama walikuwa wanavaa muzuri lakini hawakukuwa matajiri. Hata hivyo, sikuzote walionyesha kama wananihangaikia, walikuwa wananiletea zawadi ndogo-ndogo. Niliona kuwa ni Wakristo wa kweli tu ndio wanaweza kujitoa hivyo.

Nilijifunza Biblia kupitia vichapo vya Maandishi ya Vipofu. Hata kama katika akili yangu nilielewa mambo yenye nilikuwa ninajifunza, katika moyo wangu ilikuwa vigumu kukubali mambo fulani. Kwa mufano, ilikuwa vigumu kwangu kuamini kama Mungu ananihangaikia kabisa na kama watu wengine wanaweza kunihangaikia kama yeye. Nilielewa sababu gani Yehova anaacha mambo mabaya kwa muda, lakini ilikuwa vigumu kwangu kumuona kama Baba mwenye upendo kabisa. *

Pole kwa pole, mambo nilijifunza katika Maandiko yalinisaidia kubadilisha mawazo yangu. Kwa mufano, nilijifunza kama Mungu anahuzunika sana wakati anaona watu wanateseka. Juu ya watumishi wake wenye walikuwa wanateswa, Mungu alisema hivi: “Pasipo shaka nimeyaona mateso ya watu wangu . . . nayajua vizuri maumivu waliyo nayo.” (Kutoka 3:7) Wakati nilielewa sifa za muzuri za Yehova, nilichochewa kutoa maisha yangu kwake. Katika mwaka wa 1998, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova.

Pamoja na ndugu mwenye familia yake ilinikaribisha

Mwaka moja kisha kubatizwa, nilisoma masomo ya vipofu karibu na muji wa Escuintla. Muzee mumoja katika kutaniko letu aliona magumu nilikuwa ninapata ili kuenda kwenye mikutano wakati nilikuwa ninaishi katika muji wetu. Kutaniko la karibu zaidi lilikuwa kwenye milima yenye Mashahidi hao bibi na bwana walikuwa wanapitia ili kuja kunifundisha Biblia, na ilikuwa vigumu kwangu kufanya safari kama hiyo. Ili kunisaidia, muzee huyo alitafuta familia moja ya Mashahidi katika muji wa Escuintla yenye ilikuwa tayari kuishi na mimi na kunisaidia kuenda kwenye mikutano. Mupaka leo, wananihangaikia kama vile mutu wa familia yao kabisa.

Ninaweza kueleza mifano mingine mingi juu ya upendo wa kweli wenye watu wa kutaniko wamenionyesha. Mambo hayo yote yamenihakikishia kama, kuwa Shahidi wa Yehova kunanifanya nikuwe kati ya Wakristo wa kweli.—Yohana 13:34, 35.

FAIDA YENYE NIMEPATA:

Sijisikie tena kuwa mutu wa bure na mwenye hana tumaini. Sasa maisha yangu yako na kusudi kabisa. Kwa sababu niko muhubiri wa wakati wote katika kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kufundisha watu Biblia, ninakaza akili juu ya kazi ya kufundisha watu mafundisho ya muzuri sana ya Biblia kuliko kukaza akili juu ya ulemavu wangu. Tena, niko na pendeleo la kuwa muzee katika kutaniko na ninatoa hotuba za watu wote zenye kuzungumuzia Biblia katika makutaniko mbalimbali ya eneo letu. Na hata nimepata pendeleo la kutoa hotuba zenye kuzungumuzia Biblia kwenye mikusanyiko ya eneo yenye maelfu ya watu.

Ninatoa hotuba kwa kutumia Biblia yangu ya Maandishi ya Vipofu

Katika mwaka wa 2010, nilisoma Shule ya Mazoezi ya Kihuduma (leo inaitwa Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme) yenye ilifanywa katika inchi ya El Salvador. Masomo hayo yamenitayarisha ili kutimiza muzuri kazi zangu katika kutaniko. Kupata mazoezi hayo kulinifanya nijisikie kuwa Yehova Mungu ananipenda na ananiona kuwa wa maana sana. Ninaona kuwa Yehova anaweza kusaidia mutu yeyote astahili kufanya kazi yake.

Yesu alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Leo, ninaweza kusema kabisa kama niko na furaha, na hata kama sikuwazia hivyo zamani, sasa ninajisikia kuwa ninaweza kusaidia wengine.

^ fu. 13 Ili kupata habari zingine juu ya sababu zenye zinafanya Mungu aache mambo mabaya, soma sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.