Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanatoaka Sehemu ya Kumi?

Mashahidi wa Yehova Wanatoaka Sehemu ya Kumi?

 Hapana, siye Mashahidi wa Yehova hatutoake sehemu ya kumi; makuta yenye tunatumiaka mu kazi yetu ni ile yenye siye wenyewe tunatoaka kwa kujipendea. Sehemu ya kumi ni nini, na juu ya nini Mashahidi wa Yehova hawatoake sehemu ya kumi?

 Amri ya kutoa sehemu ya kumi, ilikuwa kati ya Amri zenye Yehova alipatiaka Waisraeli zamani. Lakini, Biblia inaonyesha waziwazi kama zile amri, kutia ndani amri ya “kukusanya sehemu moja za kumi,” hazihusu Wakristo leo.​—Waebrania 7:5, 18; Wakolosai 2:13, 14.

 Kuliko kutoa sehumu moja ya kumi na matoleo, Mashahidi wa Yehova wanafuata mufano wa Wakristo wa kwanza na wanafanyaka mambo mbili juu kutegemeza ya kuhubiri: Kuhubiri habari njema bila kulipwa na kutoa michango kwa kujipendea.

 Tunafuata maagizo yenye Biblia inatoa kwa Wakristo: “Kila mumoja afanye kama vile alikusudia katika moyo wake, haiko kwa kutokupenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha”​—2 Wakorinto 9:7.