WIMBO NA. 70
Tafuteni Wanaostahili
-
1. Tunapohubiri na kufundisha,
Bwana alituagiza:
‘Popote mwingiapo, tafuteni,
Wastahilio, wenye njaa.
Wasalimuni na kuwatakia,
Amani wenye kustahili.
Wengine wasipowasikiliza,
Wakung’utieni mavumbi.’
-
2. Wote wanaowapokea ninyi,
Wanampokea Bwana.
Tumaini la uzima
Litawachochea wajiunge nanyi.
Msihangaikie la kusema,
Yehova atawawezesha.
Maneno ya fadhili, yenye chumvi,
Yatawavutia wapole.
(Ona pia Mdo. 13:48; 16:14; Kol. 4:6.)