Matendo ya Mitume 13:1-52

  • Barnaba na Sauli watumwa wakiwa wamishonari (1-3)

  • Huduma huko Kipro (4-12)

  • Hotuba ya Paulo huko Antiokia ya Pisidia (13-41)

  • Amri ya kinabii ya kuwageukia watu wa mataifa (42-52)

13  Basi katika kutaniko la huko Antiokia kulikuwa na manabii na walimu:+ Barnaba, Simioni aliyeitwa Nigeri, Lukio wa Kirene, Manaeni aliyeelimishwa pamoja na Herode mtawala wa wilaya, na Sauli.  Walipokuwa wakimhudumia* Yehova* na kufunga, roho takatifu ikasema: “Wawekeni kando kwa ajili yangu Barnaba na Sauli+ kwa kazi ambayo nimewaitia.”+  Baada ya kufunga na kusali, wakaweka mikono juu yao, na kuwaacha waende.  Basi watu hao waliotumwa na roho takatifu, wakashuka kwenda Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini kwenda Kipro.  Walipofika Salami, wakaanza kulitangaza neno la Mungu katika masinagogi ya Wayahudi. Pia Yohana alikuwa pamoja nao akiwahudumia.*+  Walipokuwa wamepita katika kisiwa chote mpaka Pafo, wakakutana na mwanamume Myahudi aliyeitwa Bar-Yesu, ambaye alikuwa mlozi na nabii wa uwongo.  Alikuwa pamoja na liwali* Sergio Paulo, mwanamume mwenye akili. Akawaita Barnaba na Sauli, kwa kuwa alitamani kulisikia neno la Mungu.  Lakini Elima mlozi (kwa maana hivyo ndivyo jina lake linavyotafsiriwa) akaanza kuwapinga, akijaribu kumzuia yule liwali asiwe mwamini.  Ndipo Sauli, aitwaye pia Paulo, akiwa amejaa roho takatifu, akamtazama kwa makini 10  na kumwambia: “Ewe mtu uliyejaa kila aina ya upunjaji na kila aina ya ulaghai, wewe mwana wa Ibilisi,+ wewe adui wa kila jambo la uadilifu, je, hutaacha kuzipotosha njia za Yehova* zilizo sawa? 11  Tazama! mkono wa Yehova* uko juu yako, nawe utakuwa kipofu, hutaona nuru ya jua kwa kipindi fulani.” Mara moja akaangukiwa na ukungu mzito na giza, naye akazunguka akitafuta mtu wa kumshika mkono ili amwongoze. 12  Yule liwali alipoona jambo lililotokea, akawa mwamini kwa sababu alistaajabishwa na fundisho la Yehova.* 13  Ndipo Paulo na wenzake wakasafiri baharini kutoka Pafo na kufika Perga huko Pamfilia. Lakini Yohana+ akawaacha na kurudi Yerusalemu.+ 14  Hata hivyo, wakaendelea na safari kutoka Perga hadi Antiokia huko Pisidia. Nao wakaingia ndani ya sinagogi+ siku ya Sabato, wakaketi. 15  Baada ya kusoma hadharani Sheria+ na Manabii, maofisa wasimamizi wa sinagogi wakawatuma watu kwao, wakisema: “Wanaume, akina ndugu, ikiwa mna neno lolote la kuwatia moyo watu, lisemeni.” 16  Basi Paulo akasimama, akawapungia mkono, akasema: “Wanaume, Waisraeli nanyi wengine mnaomwogopa Mungu, sikilizeni. 17  Mungu wa watu hawa Israeli aliwachagua mababu zetu, akawainua watu hao walipokuwa wakiishi wakiwa wageni katika nchi ya Misri na kuwatoa huko kwa mkono ulioinuliwa.+ 18  Na kwa kipindi cha karibu miaka 40, akawavumilia huko nyikani.+ 19  Baada ya kuyaangamiza mataifa saba katika nchi ya Kanaani, akawapa nchi yao iwe urithi wao.+ 20  Hayo yote yalifanyika kwa karibu miaka 450. “Baada ya hapo akawapa waamuzi hadi wakati wa nabii Samweli.+ 21  Lakini baadaye wakaomba wapewe mfalme,+ na Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi, mwanamume wa kabila la Benjamini,+ kwa miaka 40. 22  Baada ya kumwondoa, akamwinua Daudi awe mfalme wao,+ na akatoa ushahidi kumhusu akisema: ‘Nimempata Daudi mwana wa Yese,+ mtu anayeupendeza moyo wangu;+ atafanya mambo yote ninayotamani.’ 23  Kama alivyoahidi, kutoka katika uzao wa* mwanamume huyu, Mungu amewaletea Israeli mwokozi, yaani, Yesu.+ 24  Kabla ya huyo kufika, Yohana alikuwa amewahubiria hadharani watu wote wa Israeli wabatizwe ili kuonyesha kwamba wametubu.+ 25  Lakini Yohana alipokuwa akimalizia huduma yake, akawa akisema: ‘Mnadhani mimi ni nani? Mimi siye. Lakini tazameni! kuna Mtu anayekuja baada yangu ambaye sistahili kuvifungua viatu vya miguu yake.’+ 26  “Wanaume, akina ndugu, ninyi wazao wa familia ya Abrahamu na wengine kati yenu mnaomwogopa Mungu, neno la wokovu huu limeletwa kwetu.+ 27  Kwa maana wakaaji wa Yerusalemu na watawala wao hawakumtambua huyo, lakini walipomhukumu walitimiza mambo yaliyosemwa na Manabii,+ ambayo husomwa kwa sauti kila sabato. 28  Ingawa hawakupata sababu ya kumuua,+ walimtaka Pilato aamuru auawe.+ 29  Walipokuwa wametimiza mambo yote yaliyoandikwa kumhusu, walimshusha kutoka kwenye mti na kumlaza kaburini.*+ 30  Lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu,+ 31  na kwa siku nyingi akaonekana na wale waliokuwa wameenda naye kutoka Galilaya hadi Yerusalemu. Sasa hao ndio mashahidi wake kwa watu.+ 32  “Basi tunawatangazia habari njema kuhusu ahadi iliyotolewa kwa mababu. 33  Mungu ameitimiza kikamili kwetu sisi, watoto wao, kwa kumfufua Yesu;+ kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: ‘Wewe ni mwanangu; leo nimekuwa Baba yako.’+ 34  Na uhakika wa kwamba Yeye alimfufua kutoka kwa wafu ili asirudi tena kwenye uharibifu, Yeye ameutaja kwa njia hii: ‘Nitawaonyesha upendo mshikamanifu, ambao ni wa uaminifu,* alioahidiwa Daudi.’+ 35  Pia, zaburi nyingine inasema: ‘Hutamruhusu mshikamanifu wako aone uharibifu.’*+ 36  Kwa upande wake, Daudi alimtumikia Mungu* katika kizazi chake mwenyewe, akalala usingizi katika kifo, akazikwa pamoja na mababu zake, naye akaona uharibifu.*+ 37  Kwa upande mwingine, yule ambaye Mungu alimfufua hakuona uharibifu.*+ 38  “Kwa hiyo, acheni ijulikane kwenu, akina ndugu, kwamba kupitia mtu huyo mnatangaziwa msamaha wa dhambi,+ 39  na kwamba mambo yote ambayo hamngetangazwa kuwa bila hatia kulingana na Sheria ya Musa,+ kila mtu anayeamini anatangazwa kuwa bila hatia kupitia mtu huyu.+ 40  Kwa hiyo, jihadharini ili msipatwe na mambo haya yanayosemwa katika Manabii: 41  ‘Tazameni, ninyi wenye dharau, na mshangae na kuangamia, kwa sababu ninafanya kazi fulani katika siku zenu, kazi ambayo hamtaiamini kamwe hata mtu yeyote akiwaeleza kirefu.’”+ 42  Basi walipokuwa wakiondoka, watu wakawasihi wazungumzie mambo hayo Sabato iliyofuata. 43  Baada ya kusanyiko la sinagogi kumalizika, Wayahudi wengi na wageuzwa imani waliomwabudu Mungu wakawafuata Paulo na Barnaba, ambao walisema nao na kuwahimiza waendelee kubaki katika fadhili zisizostahiliwa za Mungu.+ 44  Sabato iliyofuata karibu jiji lote lilikusanyika ili kulisikia neno la Yehova.* 45  Wayahudi walipouona umati, walijawa na wivu wakaanza kupinga wakikufuru mambo ambayo Paulo alikuwa akisema.+ 46  Kisha Paulo na Barnaba wakawaambia hivi kwa ujasiri: “Ilikuwa lazima neno la Mungu lihubiriwe kwenu kwanza.+ Kwa kuwa mnalikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, tazameni! tunawageukia mataifa.+ 47  Kwa maana Yehova* ametuamuru kwa maneno haya: ‘Nimewachagua muwe nuru ya mataifa, na muwe wokovu mpaka miisho ya dunia.’”+ 48  Watu wa mataifa waliposikia jambo hilo, wakaanza kushangilia na kulitukuza neno la Yehova,* na wote waliokuwa na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele wakawa waamini. 49  Zaidi ya hayo, neno la Yehova* lilikuwa likienezwa katika nchi yote. 50  Lakini Wayahudi wakawachochea wanawake mashuhuri waliomwogopa Mungu, na wakuu wa jiji, nao wakaanza kuwatesa+ Paulo na Barnaba na kuwatupa nje ya mipaka yao. 51  Basi wakawakung’utia mavumbi yaliyokuwa kwenye miguu yao na kwenda Ikoniamu.+ 52  Nao wanafunzi wakaendelea kujawa na shangwe+ na roho takatifu.

Maelezo ya Chini

Au “wakimhudumia hadharani.”
Au “akiwasaidia”
Gavana Mroma aliyesimamia mkoa. Angalia Kamusi.
Tnn., “mbegu ya.”
Au “kwenye kaburi la ukumbusho.”
Au “wenye kutegemeka.”
Au “aoze.”
Au “alifanya mapenzi ya Mungu.”
Au “na mwili wake ukaoza.”
Au “hakuoza.”