Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Wanajaribu Kujipatia Wokovu kwa Kuhubiri Nyumba kwa Nyumba?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanajaribu Kujipatia Wokovu kwa Kuhubiri Nyumba kwa Nyumba?

 Hapana. Tunashiriki kwa ukawaida katika kazi yetu ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, lakini hatuamini kwamba tunajipatia wokovu kwa kufanya kazi hiyo. (Waefeso 2:8) Kwa nini?

 Fikiria ulinganisho huu: Wazia mtu fulani mwema aliahidi kutoa zawadi yenye thamani kwa kila mtu atakayefika mahali fulani tarehe fulani. Ikiwa kwa kweli uliamini ahadi ya mtu huyo, je, usingefuata maagizo yake? Bila shaka ungeyafuata! Yaelekea, ungewaambia rafiki zako na familia yako pia kuhusu fursa hiyo, ili wao pia wafaidike. Hata hivyo, hutapata zawadi kwa kufuata maagizo ya mtu huyo. Zawadi bado ni zawadi tu.

 Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wanaamini ahadi ya Mungu ya uzima wa milele kwa wote wanaomtii. (Waroma 6:23) Tunajitahidi kuwaambia wengine mambo tunayoamini, tukitumaini kwamba watafaidika na ahadi za Mungu. Lakini hatuamini kwamba tunajipatia wokovu kwa kufanya kazi hiyo. (Waroma 1:17; 3:28) Kwa kweli, hakuna jambo lolote ambalo mtu anaweza kufanya linaloweza kumfanya astahili kupokea baraka kubwa kama hiyo kutoka kwa Mungu. “Alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali kwa sababu ya huruma yake.”—Tito 3:5, Biblia Habari Njema.