Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JW LIBRARY

Tafuta Katika Biblia au Chapisho​—Windows

Tafuta Katika Biblia au Chapisho​—Windows

Sehemu ya kutafuta ya JW Library inakuruhusu upate neno au fungu la maneno katika Biblia au chapisho.

Fuata maelekezo yafuatayo ili kutumia sehemu ya kutafuta:

 Tafuta Katika Biblia

Unaweza kutafuta neno au fungu la maneno katika Biblia unayosoma.

Ikiwa umefungua Biblia, bofya kisanduku cha Tafuta; kisha anza kuandika neno unalotafuta. Unapoandika utaona mapendekezo kadhaa. Bofya pendekezo moja au ubofye kitufe cha Nenda kwenye kibodi ili uone matokeo.

Sehemu ya Maandiko Makuu inakuonyesha jinsi mistari inayotumiwa mara nyingi inavyotumia neno unalotafuta. Sehemu iliyoandikwa Mistari Yote inaonyesha mistari yote iliyo na neno unalotafuta ikiwa imepangwa kulingana na mfuatano wa vitabu vya Biblia. Sehemu iliyoandikwa Makala inaonyesha makala kwenye utangulizi na kwenye fahirisi zilizo na neno unalotafuta.

Ikiwa unatafuta maneno kadhaa, tia alama kisanduku Patanisha Maneno Kikamili ili programu itafute maneno kwa mpangilio uleule kama ulivyoyaandika.

 Tafuta Katika Chapisho

Unaweza kutafuta neno au fungu la maneno katika chapisho unalosoma.

Ikiwa umefungua chapisho, bofya kisanduku cha Tafuta; kisha anza kuandika neno unalotaka kupata. Unapoandika utaona mapendekezo kadhaa. Bofya pendekezo moja au ubofye kitufe cha Nenda kwenye kibodi ili uone matokeo.

Ikiwa unatafuta maneno kadhaa, tia alama kisanduku Patanisha Maneno Kikamili ili programu itafute maneno kwa mpangilio uleule kama ulivyoyaandika.

 Tafuta Habari Kuu

Ikiwa umepakua kitabu Insight on the Scriptures, unaweza kutafuta habari kuu. Unaweza kutumia sehemu hii unaposoma Biblia au chapisho lolote katika programu hii.

Bofya kisanduku cha Tafuta; kisha anza kuandika habari kuu unayotaka kupata. Unapoandika, habari kuu katika kitabu Insight on the Scriptures zitatiwa ndani ya orodha ya mapendekezo. Bofya habari kuu ili ufungue makala.

Sehemu hizo mbalimbali zilipatikana Oktoba 2014 kwenye JW Library toleo la 1.3.4, ambalo linafanya kazi vizuri kwenye vifaa vinavyotumia mfumo wa Windows 8.0 au wa karibuni zaidi. Ikiwa huoni mambo haya, tafadhali fuata mwelekezo kwenye makala “Anza Kutumia JW Library​—Windows,” kwenye Pata Habari za Karibuni Zaidi.