Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NJIA YA MAISHA YENYE FURAHA

Kusudi Katika Maisha

Kusudi Katika Maisha

SISI WANADAMU TUKO WA PEKEE KATIKA NJIA NYINGI​—TUNAANDIKA, TUNACHORA, TUNATOKEZA VITU, NA TUNAFIKIRIA MAULIZO YA MAANA KUHUSU MAISHA: Sababu gani ulimwengu uko? Namna gani tulifikia kuwako? Maisha yako na kusudi gani? Wakati wenye kuja utakuwa namna gani?

Watu fulani wanaepuka kuuliza maulizo hayo, wanawaza kuwa majibu ya maulizo hayo yako nguvu sana kuelewa. Wengine wanasema kwamba maulizo hayo hayana maana kwa sababu uzima ulijitokeza tu wenyewe. Mwalimu mumoja wa historia na biolojia mwenye kuitwa William Provine alisema, “Hakuna miungu, hakuna kusudi.” Aliongeza hivi: “Hakuna musingi wenye nguvu wa kanuni, hakuna pia kusudi la maana katika maisha.”

Lakini, watu fulani hawakubaliane na mawazo ya kwamba hakuna Mungu na kwamba maisha hayana kusudi. Wanaona kuwa ulimwengu ni wenye kuongozwa na sheria zenye kupangwa muzuri. Wanashangazwa na uumbaji wenye umefanywa kwa njia ya ajabu, uumbaji wenye wanadamu wanajaribu kuiga ili kutengeneza vitu mbalimbali. Na mambo yenye wanavumbua kila siku yanawahakikishia kwamba uumbaji huo wa hali ya juu na wenye kushangaza haukujitokeza wenyewe tu, lakini ulitokezwa na Muumbaji mwenye akili.

Mawazo kama hayo yamechochea watu wenye kuamini mageuzi, wachunguze tena namna yao ya kufikiri. Tuzungumuzie mifano mbili.

MUPASUAJI WA MISHIPA YA UBONGO DR. ALEXEI MARNOV. Alisema hivi: “Masomo kwenye nilisomea, tulifundishwa kwamba hakuna Mungu na kwamba vitu vilijitokeza vyenyewe. Mutu yeyote mwenye aliamini Mungu, alionwa kama vile mutu mwenye kuwa na akili kidogo.” Lakini, katika mwaka wa 1990, mawazo yake yalianza kubadilika.

Anaeleza hivi: “Sikuzote nimejikaza kuelewa sababu yenye kupatana na akili yenye kufanya vitu fulani vikuwe, kutia ndani ubongo. Tunaelewa sababu yenye inafanya kiungo hiki cha ajabu sana kionwe kuwa kiungo chenye kuwa nguvu zaidi kueleweka katika ulimwengu wetu. Lakini, ubongo ulifanywa tu ili usaidie mutu kupata ujuzi na ufundi mbalimbali na kisha akufe? Hilo lilionekana kuwa halina maana, halikupatana na akili. Kwa hiyo, nilianza kujiuliza: ‘Sababu gani tuko katika ulimwengu? Maisha yako na kusudi gani?’ Kisha kuwaza sana, nilifikia kuona kwamba kunapaswa kuwa Muumbaji.”

Kutafuta kusudi la maisha kulimuchochea Alexei achunguze mambo yenye Biblia inafundisha. Kisha wakati fulani, bibi yake mwenye alikuwa munganga, mwenye naye aliamini kwamba hakuna Mungu, alijifunza pia Biblia​—alifanya hivyo kwanza ili kuonyesha bwana yake kuwa alikamata uamuzi wa mubaya! Lakini, sasa, wote wawili wanaamini kabisa kwamba Mungu iko na wanaelewa kusudi la Mungu kuhusu wanadamu kama vile imeonyeshwa katika Biblia.

DR. HUABI YIN alijifunza fizikia (physique), na kwa miaka mingi alifanya uchunguzi kuhusu jua.

Anasema, “Wakati wowote sisi wanasayansi tunajifunza kuhusu mambo ya asili, tunaona kwamba yamepangwa kwa utaratibu wa hali ya juu, na hilo ni kwa sababu kuko sheria zenye kupangwa muzuri. Nilijiuliza, ‘Sheria hizo zilitokea namna gani? Ikiwa hata moto kidogo tu wenye tunatumia ili kupika chakula unapaswa kulindwa muzuri, sasa, ni nani mwenye aliweka sheria zenye kuongoza jua?’ Kisha, nilifikia kuona kuwa maneno yenye kupatikana mwanzoni mwa andiko la kwanza katika Biblia, ni jibu lenye kupatana na akili: ‘Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.’”​—Mwanzo 1:1.

Ni kweli kwamba sayansi imesaidia watu kupata majibu ya maulizo mengi kama vile: Namna gani chembe za ubongo zinatumika? Na namna gani jua linatokeza mwangaza na joto? Lakini kama vile Alexei na Huabi walivumbua, Biblia inatoa majibu ya maulizo ya maana zaidi kama vile: Sababu gani ulimwengu uko? Sababu gani unaongozwa na sheria? Na sababu gani tunaishi?

Kuhusu dunia, Biblia inasema hivi: “[Mungu] hakuiumba tu bila sababu, aliiumba ili ikaliwe na watu.” (Isaya 45:18) Kwa kweli, Mungu iko na kusudi juu ya dunia, na kama vile habari yenye kufuata itaonyesha, kusudi hilo linapatana kabisa na tumaini letu juu ya wakati wenye kuja.