Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tendo Moja la Wema wa Kikristo

Tendo Moja la Wema wa Kikristo

KATIKA muji mudogo wa Gujarati, India, baba ya John alibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova kumepita miaka 60. John na ndugu na dada zake watano pamoja na mama yao, wote walikuwa wanaamini sana dini ya Katoliki ya Roma; kwa hiyo, walipinga imani ya baba yao.

Siku moja baba ya John alimuomba apelekee rafiki yake wa kutaniko lake barua fulani. Lakini, asubuhi hiyo John alijiumiza sana kwenye kidole chake wakati alikuwa anafungua chombo kikubwa cha chuma. Hata hivyo, kwa sababu alipenda kutii baba yake, alifunga kitambaa kwenye kidonda chake chenye kuvuya damu na akatembea kwa miguu ili kupeleka barua hiyo.

Wakati alifika mahali alikuwa ametumwa, bibi ya rafiki huyo wa baba yake, mwenye alikuwa Shahidi wa Yehova alipokea barua hiyo. Aliona kidole cha John chenye kuumia na akajitolea kumusaidia. Alitafuta chombo chake cha kuwekea dawa za matunzo ya haraka, akasafisha kidonda hicho kwa kutumia dawa ya kuua mikrobe, na akafunga kwenye kidole hicho kitambaa cha kufunga kidonda. Kisha akapikia John chai ya moto, na wakati huo wote alikuwa anazungumuza naye kwa upole juu ya Biblia.

Wakati huo, ubaguzi wa John juu ya Mashahidi wa Yehova ukaanza kupunguka, kwa hiyo alimuuliza juu ya mafundisho yao mawili yenye kuwa tofauti na mambo yenye baba yake anaamini, ikiwa Yesu ni Mungu na ikiwa Wakristo wanapaswa kusali kwa Maria. Kwa sababu alikuwa amejifunza Gujarati, luga ya kizalikio ya John, Shahidi huyo alimujibia kwa kutumia Biblia na akamupatia kijitabu “Habari Njema Hizi za Ufalme.”

Kisha wakati John alisoma kijitabu hicho, aliona kuwa ni mara yake ya kwanza kusikia kweli ya Biblia. Alienda kwa padri wao na kumuuliza maulizo hayo mawili. Mara moja padri alikasirika sana na akamutupia Biblia, na kumuambia hivi kwa hasira: “Umekuwa Shetani! Unionyeshe ni wapi Biblia inasema kama Yesu haiko Mungu. Unionyeshe wapi inasema kuwa haupaswe kuabudu Maria. Unionyeshe!” John alihuzunishwa na namna padri huyo alitenda, na akamuambia hivi: “Sitaingiaka tena katika kanisa Katoliki.” Na hakuingiaka tena!

John alianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, alikubali ibada ya kweli, na alianza kumutumikia Yehova. Kisha wakati fulani, watu fulani wa familia yake walifanya hivyo pia. Leo, John angali na alama ya kidonda hicho kwenye kidole chake cha mukono wa kuume kwenye alijikata kumepita miaka 60 hivi. Anakumbuka kwa furaha tendo moja la wema wa Kikristo lenye lilimuchochea aanze kumutumikia Yehova.​—2 Kor. 6:4, 6.