Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yosefu wa Arimathea Anakamata Musimamo

Yosefu wa Arimathea Anakamata Musimamo

YOSEFU WA ARIMATHEA hakujua kama atapata ujasiri wa kuonana na gavana Muroma. Pontio Pilato alijulikana kuwa mutu mwenye kuwa na moyo mugumu sana. Lakini, ili Yesu azikwe kwa njia ya heshima, mutu fulani alipaswa kumuomba Pilato ruhusu ya kuchukua mwili wake. Kulingana na namna mambo yalitendeka, haikuwa vigumu kuonana naye moja kwa moja kama vile pengine Yosefu alikuwa amewazia. Kisha ofisa fulani kumuhakikishia kuwa Yesu alikuwa amekufa, Pilato alikubali ombi hilo. Hata kama alikuwa angali na huzuni, Yosefu alirudia haraka mahali penye Yesu aliuawa.​—Mk. 15:42-45.

  • Yosefu wa Arimathea alikuwa nani?

  • Alikuwa na uhusiano gani pamoja na Yesu?

  • Na sababu gani tunapaswa kupendezwa na habari yake?

ALIKUWA KATIKA SANHEDRINI

Injili ya Marko yenye kuongozwa na roho ya Mungu inamuita Yosefu kuwa ‘mushiriki wa Baraza mwenye kusifika.’ Katika hali hii, Baraza hilo linaweza tu kuwa Sanhedrini, tribinali kubwa na baraza kubwa zaidi la usimamizi la Wayahudi. (Mk. 15:1, 43) Yosefu alikuwa kati ya viongozi wa Wayahudi, kwa hiyo tunaelewa sababu gani angeweza kupata ruhusa ya kuonana na gavana Muroma. Haishangaze kujua kuwa Yosefu alikuwa pia tajiri.​—Mt. 27:57.

Uko na ujasiri wa kuonyesha waziwazi kuwa Yesu ni Mufalme wako?

Kwa ujumla, watu wenye walikuwa katika Sanhedrini walimuchukia Yesu. Walipanga njama ya kumuua. Lakini, Yosefu anaitwa kuwa ‘mutu mwema na muadilifu.’ (Lu. 23:50) Tofauti na watu wengi wenye walikuwa katika Sanhedrini, Yosefu alikuwa muaminifu katika maisha yake na alijikaza sana kutii amri za Mungu. Pia ‘alikuwa anangojea ufalme wa Mungu,’ hilo linaweza kuonyesha sababu gani alifikia kuwa mwanafunzi wa Yesu. (Mk. 15:43; Mt. 27:57) Pengine, alipenda ujumbe wa Yesu kwa sababu aliona kweli na haki kuwa mambo ya maana.

MWANAFUNZI WA SIRI

Andiko la Yohana 19:38 linasema kuwa Yosefu ‘alikuwa mwanafunzi wa Yesu lakini kwa siri kwa sababu alikuwa anawaogopa Wayahudi.’ Yosefu alikuwa anaogopa nini? Alijua namna Wayahudi walimuchukia Yesu na namna waliazimia kabisa kufukuza katika sinagogi mutu yeyote mwenye angeonyesha waziwazi kuwa anamuamini. (Yoh. 7:45-49; 9:22) Ikiwa mutu angefukuzwa katika sinagogi, angezarauliwa, angeepukwa, na kutendewa na Wayahudi wenzake kama mutu mwenye kutengwa. Kwa hiyo, Yosefu alisita kuonyesha waziwazi kuwa alimuamini Yesu. Ikiwa angefanya hivyo angepoteza cheo chake na heshima yake.

Wengine walikuwa katika hali kama ile ya Yosefu. Yohana 12:42 inasema kuwa ‘wengi hata kati ya watawala kwa kweli walimuamini [Yesu], lakini kwa sababu ya Mafarisayo wakawa hawamukiri [hawaonyeshe waziwazi], ili wasifukuzwe katika sinagogi.’ Mutu mwengine mwenye alikuwa pia katika hali hiyo, ni Nikodemo, mwenye alikuwa pia katika Sanhedrini.​—Yoh. 3:1-10; 7:50-52.

Hata hivyo, Yosefu alikuwa mwanafunzi, lakini hangeweza kusema jambo hilo waziwazi. Hilo lilikuwa tatizo kubwa, zaidi sana kulingana na maneno haya ya Yesu: ‘Kila mutu anayekiri [anayenikubali] mbele ya wanadamu kwamba yuko katika umoja pamoja nami, mimi pia nitakiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni kwamba niko katika umoja pamoja naye. Lakini yeyote yule anayenikana mimi mbele ya watu, mimi pia nitamukana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.’ (Mt. 10:32, 33) Yosefu hakumukana Yesu, lakini hakupata pia ujasiri wa kuonyesha waziwazi kuwa anamuamini. Wewe unaonyesha waziwazi kuwa unamuamini?

Yosefu alifanya jambo fulani la muzuri, Biblia inaonyesha kuwa hakuunga mukono njama ya Sanhedrini ya kumuua Yesu. (Lu. 23:51) Pengine, kama vile wengine wanasema, Yosefu hakukuwa pale wakati Yesu alikuwa anasambishwa. Hata iwe mambo yalikuwa hivyo ao hapana, Yosefu alipaswa kuhuzunishwa sana kwa sababu ya ukosefu huo mubaya sana wa haki; lakini hangeweza kufanya jambo lolote ili kuzuia jambo hilo!

ANASHINDA WOGA

Kufikia wakati Yesu alikufa, ni wazi kuwa Yosefu alikuwa ameshinda woga wake, na akaamua kuunga mukono wanafunzi wa Yesu. Uamuzi huo unaonekana katika maneno yenye kuwa kwenye Marko 15:43, inasema hivi: “Akajipa moyo kuingia mbele ya Pilato na kuomba apewe mwili wa Yesu.”

Inaonekana kuwa Yosefu alikuwa hapo wakati Yesu alikufa. Kwa kweli, alijua kuwa Yesu alishakufa mbele ya gavana Pilato kupata habari hiyo. Kwa hiyo, wakati Yosefu aliomba mwili wa Yesu, gavana huyo “akataka kujua kama tayari alikuwa amekufa.” (Mk. 15:44) Ikiwa Yosefu aliona maumivu ya Yesu kwenye muti wa mateso, pengine hilo lilimuchochea achunguze zamiri yake na mwishowe akaamua kuwa anapaswa kuonyesha waziwazi kuwa alikuwa mwanafunzi wa Yesu. Iwe ilikuwa hivyo ao hapana, sasa Yosefu alichochewa kutenda. Hangekuwa tena mwanafunzi wa siri.

YOSEFU ANAMUZIKA YESU

Sheria ya Wayahudi ilisema kuwa wale wenye kuhukumiwa kifo walipaswa kuzikwa mbele ya jua kutua. (Kum. 21:22, 23) Lakini, Waroma hawakuhangaikia jambo hilo, maiti ya watu wabaya wenye walikuwa wameuawa ilikuwa inaachwa kwenye muti ili ioze ao ilikuwa inatupwa katika kaburi la watu wengi. Lakini Yosefu hakukuwa na mawazo hayo juu ya Yesu. Karibu na mahali penye Yesu aliuawa, Yosefu alikuwa na kaburi mupya lenye lilikuwa limechongwa katika mwamba. Kwa sababu kaburi hilo lilikuwa mupya, hilo linaonyesha kwamba Yosefu alikuwa ametoka tu Arimathea * na kuhamia Yerusalemu na kwamba alipanga kutumia mahali hapo kuwa nafasi ya kuzikia watu wa familia yake. (Lu. 23:53; Yoh. 19:41) Yosefu alionyesha ukarimu kwa kumuzika Yesu katika kaburi lenye yeye mwenye angezikwa ndani wakati wenye kuja na hilo lilitimiza unabii wenye kuonyesha kuwa Masiya angezikwa pamoja na “matajiri.”​—Isa. 53:5, 8, 9.

Kuko jambo lolote lenye unaona kuwa la maana zaidi kuliko uhusiano wako pamoja na Yehova?

Injili zote ine zinasema kuwa kisha mwili wa Yesu kuondolewa kwenye muti, Yosefu aliufunga katika kitambaa cha kitani kizuri na kuuweka katika kaburi lake mwenyewe. (Mt. 27:59-61; Mk. 15:46, 47; Lu. 23:53, 55; Yoh. 19:38-40) Mutu mumoja tu mwenye anatajwa kuwa alisaidia Yosefu ni Nikodemo, mwenye alileta marashi ya kutumia wakati maziko. Kwa sababu wanaume hao wawili walikuwa wenye mamlaka, inawezekana kuwa hawangebeba mwili huo wao wenyewe. Inawezekana kabisa kuwa walitumia watumishi wao ili wabebe mwili huo na kuuzika. Hata kama walitumia watumishi, kazi yenye wanaume hao walifanya ilikuwa ya maana sana. Mutu yeyote mwenye alikuwa amegusa maiti alipaswa kubakia asiye safi kwa kipindi cha siku saba. (Hes. 19:11; Hag. 2:13) Kuwa katika hali hiyo kungewaomba wasikaribie wengine katika juma la Pasaka na wakose kufanya sherehe zote za Pasaka. (Hes. 9:6) Kwa kufanya mipango ili Yesu azikwe, Yosefu pia angezarauliwa na wanaume wenzake wa Sanhedrini. Lakini, wakati huo alikuwa tayari kukubali mambo yenye yangemupata kwa sababu ya kumuzika Yesu kwa njia ya heshima na kuonyesha waziwazi kuwa alikuwa mwanafunzi wa Kristo.

MWISHO WA HABARI JUU YA YOSEFU

Kisha Yesu kuzikwa, Biblia haitaje tena Yosefu wa Arimathea, na hilo linafanya tujiulize hivi: Alipatwa na nini? Kwa kweli, hatujue. Lakini, kulingana na mambo yenye tumezungumuzia, inawezekana kabisa kuwa alionyesha waziwazi kwamba alikuwa Mukristo. Kwa kweli, wakati wa majaribu na magumu, imani na ujasiri wake vilikuwa vinaongezeka kuliko kupunguka. Hiyo ilikuwa alama ya muzuri.

Habari hii inatokeza ulizo lenye sisi wote tunapaswa kufikiria: Kuko jambo lolote, kama vile cheo, kazi, vitu vya kimwili, upendo wa familia, ao hata uhuru wetu, lenye tunaona kuwa la maana zaidi kuliko uhusiano wetu pamoja na Yehova?

^ fu. 18 Pengine Arimathea inaitiwa pia Rama, ilikuwa katika eneo la leo la Rentis (Rantis). Nabii Samweli alizaliwa katika eneo hilo, lenye lilipatikana kwenye umbali wa kilometre 35 hivi, kaskazini-mangaribi ya Yerusalemu.​—1 Sam. 1:19, 20.