Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kupiganisha Hali ya Kujisikia Kuwa Hauko Salama

Namna ya Kupiganisha Hali ya Kujisikia Kuwa Hauko Salama

MUTOTO mwenye kutoka tu kuzaliwa ndiye mwenye kuonekana zaidi kuwa hana uwezo wowote. Wakati tulizaliwa, usalama wetu wote ulikuwa katika mikono ya wazazi wetu. Wakati tulijifunza kutembea, tuliona kama watu wenye walituzunguka walikuwa warefu kuliko sisi. Kama wazazi wetu hawakukuwa karibu, watu hao walituogopesha sana. Lakini tulijisikia kuwa salama wakati tulikamata mukono wa baba ao wa mama yetu.

Wakati tulikuwa watoto, wazazi wetu walituonyesha upendo na walitutia moyo, jambo hilo ndilo lilifanya tujisikie muzuri. Wakati tuliona kama wazazi wetu walitupenda, tulijisikia kuwa salama zaidi. Tulijisikia wenye uhakika zaidi na tulifanya maendeleo, wakati walituhakikishia kama tulikuwa tunafanya muzuri.

Wakati tulikomaa kidogo, marafiki wetu wa sana walitufanya pia tujisikie kuwa salama. Tulijisikia muzuri wakati tulikuwa nao, na walifanya tusiogope sana kwenye masomo.

Kwa kweli, mawazo hayo yanaonyesha namna maisha ya utoto yalikuwa. Vijana fulani hawapate marafiki wengi wa sana, na watoto wengi hawapate musaada kabisa kutoka kwa wazazi wao. Melissa * anasema hivi: “Wakati ninaona picha za watu wa familia wenye umoja wakifanya mambo pamoja, ninajiambia, ‘Mimi pia ningeishi hivyo wakati nilikuwa mutoto!’” Pengine na wewe unajisikia namna hiyo.

MAGUMU YA KUKOMAA KATIKA HALI YENYE HAINA USALAMA

Pengine haukujisikia salama wakati ulikuwa mutoto. Labda, haukuonyeshwa upendo mwingi na haukutiwa moyo sana. Inawezekana unakumbuka ugomvi wenye ulikuwa wa kawaida kati ya wazazi wako na namna jambo hilo lilifanya ndoa yao ivunjike, pengine uliwaza kimakosa kama ni wewe ulifanya jambo hilo litokee. Na jambo la mubaya zaidi, pengine baba ao mama yako alikuwa anakutukana ao kukupiga sana.

Mutoto mwenye kujisikia kuwa hana usalama anaweza kutenda namna gani? Hilo linafanya watoto fulani watumie dawa za kulewesha ao kunywa pombe sana katika miaka yao ya ujana. Wengine wanajiunga na vikundi vya watenda-mabaya ili wajisikie kama wanapendwa. Vijana wenye hawajisikie kuwa salama wanaanzisha haraka urafiki wa kimapenzi, ili kupendwa kutafuta na kuhangaikiwa. Lakini, kwa kawaida urafiki huo hauendelee kwa muda murefu, na wakati unavunjika, mara nyingi hilo linafanya wakose usalama zaidi.

Vijana wenye kukosa usalama ambao wanaepuka mambo hayo ya mubaya, nao pia wanaweza kukomaa na mawazo ya kujisikia kuwa hawako wa maana kabisa. Ana anaeleza hivi: “Nilifikia kuamini kama nilikuwa mutu wa bure, kwa sababu mama yangu alikuwa ananiambia jambo hilo tena na tena. Sikumbuke hata siku yenye alinipongeza ao kunionyesha upendo.”

Haiko tu namna watu walikomaa ndiyo inafanya wajisikie kuwa hawako salama. Tunaweza kujisikia kuwa hatuko salama kwa sababu ya kuvunjika kwa ndoa katika njia yenye kuumiza, magumu ya uzee, ao hata kwa sababu ya kuhangaikia sura yetu. Hata kama ni juu ya sababu gani, kujisikia kuwa hatuko salama kunaweza kutufanya tukose furaha na kunaweza kuharibisha urafiki wetu pamoja na wengine. Tunaweza kufanya nini ili kupiganisha hali hiyo?

MUNGU ANATUHANGAIKIA

Ni lazima tujue kama kuko musaada. Sisi wote tuko na mutu mwenye anaweza kutusaidia na mwenye anataka kutusaidia, ni kusema, Mungu mwenyewe.

Mungu alitoa ujumbe huu kupitia nabii Isaya: ‘Usiogope, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu. Nitakusaidia kwelikweli. Nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa uadilifu [haki].’ (Isaya 41:10, 13) Ni jambo lenye kutuliza moyo kujua kama, kwa njia ya mufano, Mungu anapenda kutushika mukono! Hatuna sababu ya kuhangaika!

Biblia inazungumuzia waabudu wa Mungu wenye walihangaika lakini walijifunza kushika mukono wa Mungu. Hana, mama ya Samweli, alijisikia kuwa mutu wa bure, kwa sababu alikuwa tasa. Mara nyingi alizarauliwa kwa sababu ya jambo hilo. Hilo lilifanya apoteze hamu ya kula na alilia mara nyingi. (1 Samweli 1:6, 8) Lakini wakati alimuambia Mungu namna alikuwa anajisikia, hakuendelea kuwa na huzuni tena.—1 Samweli 1:18.

Daudi, muandikaji wa zaburi, alijisikia pia wakati fulani kuwa hakukuwa na usalama. Kwa miaka mingi, Mufalme Sauli alijaribu kumuwinda. Daudi aliponyoka mara nyingi wakati Sauli alitaka kumuua, na wakati fulani alijisikia kuwa anazama katika magumu yake. (Zaburi 55:3-5; 69:1) Hata kama alikuwa katika hali hiyo, aliandika hivi: ‘Nitajilaza na kulala usingizi, kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, unanifanya nikae kwa usalama.’—Zaburi 4:8.

Hana na Daudi, wote wawili, walimuambia Yehova namna walikuwa wanajisikia na waliona kama aliwasaidia. (Zaburi 55:22) Namna gani tunaweza kufanya kama wao leo?

MAMBO TATU YA KUFANYA ILI KUJISIKIA SALAMA ZAIDI

1. Ujifunze kutumainia Yehova kama Baba.

Yesu alituomba tumujue Baba yake, “Mungu wa pekee wa kweli.” (Yohana 17:3) Mutume Paulo anatuhakikishia kama ‘haiko mbali sana na kila mumoja wetu.’ (Matendo 17:27) Yakobo aliandika hivi: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’—Yakobo 4:8.

Kujua kama tuko na Baba wa mbinguni mwenye anatupenda na mwenye anatuhangaikia, ni jambo la maana sana ili kupiganisha mahangaiko. Kwa kweli, inaomba wakati ili kuwa na tumaini hilo, lakini watu wengi wamevumbua kama kufanya hivyo kunasaidia kabisa. Caroline anasema hivi: “Wakati nilianza kumuona Yehova kama Baba yangu, nilifikia kupata mutu mwenye ningeweza kuambia namna nilijisikia katika moyo. Jambo hilo lilinituliza sana!”

Rachel anakumbuka hivi: “Yehova ndiye alinisaidia kujisikia salama wakati nilibakia mimi peke bila wazazi. Ningeweza kuzungumuza naye na kumuomba musaada. Na alinisaidia.” *

2. Utafute familia ya kiroho.

Yesu alifundisha wanafunzi wake waonane kuwa ndugu na dada. Aliwaambia hivi: ‘Ninyi wote ni ndugu.’ (Mathayo 23:8) Alipenda wanafunzi wake wa kweli wapendane kati yao na wafanyize familia kubwa ya kiroho.—Mathayo 12:48-50; Yohana 13:35.

Kwa kweli, makutaniko ya Mashahidi wa Yehova ni familia ya kweli ya kiroho kwenye watu wanapata furaha na kitulizo. (Waebrania 10:24, 25) Watu wengi wameona kama mikutano ya kutaniko ni kama dawa ya kupaka yenye kuponyesha vidonda vyao vya moyoni.

Eva anakumbuka hivi: “Katika kutaniko letu nilikuwa na rafiki wa kweli, mwenye alielewa magumu yangu. Alinisikiliza, alinisomea Biblia, na kusali pamoja na mimi. Alifanya yake yote ili nisijisikie kuwa peke yangu. Alinisaidia kuzungumuzia mambo kwa undani na kujiondolea muzigo. Kupitia musaada wake, nilianza kujisikia kuwa na usalama zaidi.” Rachel anaongezea hivi: “Nilipata ‘mama na baba’ katika kutaniko. Kwa kweli, walifanya nijisikie salama na mwenye kupendwa.”

3. Uonyeshe wengine upendo na wema.

Kuwaonyesha wengine upendo na wema kunasaidia kufanya marafiki wa kweli. Yesu alisema hivi: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Na kwa kweli, tutaona kama tukionyesha wengine upendo mwingi, watatuonyesha pia upendo mwingi. Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: ‘Mukuwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi’.—Luka 6:38.

Ikiwa tunaonyesha na kuonyeshwa upendo, tunajisikia kuwa salama zaidi. Kama vile Biblia inaonyesha, ‘upendo haushindwe kamwe.’ (1 Wakorintho 13:8) María anasema hivi: “Ninajua kama mawazo fulani ya mubaya yenye niko nayo juu yangu hayako ya kweli. Ninapiganisha mawazo hayo ya mubaya kwa kuwasaidia wengine na kwa kujisahau mimi mwenyewe. Sikuzote, ninasikia furaha wakati ninafanya jambo fulani kwa ajili ya wengine.”

USALAMA KWA WATU WOTE

Mambo yenye tunataja hapo juu haiko ‘dawa ya muujiza’ yenye kuleta palepale kitulizo cha kuendelea. Lakini, yanaweza kusaidia sana. Caroline anasema hivi: “Ningali ninajisikia kuwa mwenye kukosa usalama. Lakini sasa ninajiona kuwa wa maana. Ninajua kama Mungu ananihangaikia, na niko na marafiki wengi wa sana wenye kunifanya pia nijisikie salama.” Rachel naye anajisikia hivyo. Anasema hivi: “Mara kwa mara, ninasikia huzuni nyingi. Lakini niko na ndugu na dada wa kiroho wenye ninaweza kuomba mashauri na wenye wananisaidia kuwa na mawazo ya muzuri. Na zaidi ya hilo, niko na Baba wa mbinguni mwenye ninazungumuza naye kila siku. Mambo hayo yananisaidia sana.”

Biblia inazungumuzia dunia mupya na katika dunia hiyo, watu wote watajisikia kuwa salama

Tena, kuko jambo lenye litamaliza milele hali ya kukosa usalama. Biblia inazungumuzia dunia mupya na katika dunia hiyo, watu wote watajisikia kuwa salama. Neno la Mungu linaahidi hivi: ‘Wataketi [watakaa], kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya mutini wake, wala hakutakuwa na mutu yeyote anayewatetemesha.’ (Mika 4:4) Wakati huo hakuna mutu atatukosesha usalama, ao kutufanya mubaya. Hata mambo ya kuhuzunisha sana ya wakati uliopita “hayataingia moyoni.” (Isaya 65:17, 25) Mungu na Kristo Yesu, Mwana wake, wataleta “uadilifu [haki] wa kweli.” Jambo hilo litatokeza ‘utulivu na usalama mupaka wakati usio na kipimo.’—Isaya 32:17.

^ fu. 5 Majina yote yamebadilishwa.

^ fu. 21 Mashahidi wa Yehova wanajifunza Biblia bila kulipa pamoja na watu wenye wanapenda kumukaribia Mungu zaidi.