Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Misiba ya Asili​—Je, Inaonyesha Kama Mungu Hana Huruma?

Misiba ya Asili​—Je, Inaonyesha Kama Mungu Hana Huruma?

MAMBO AMBAYO WATU WANASEMA: “Mungu ndiye anatawala ulimwengu, kwa hiyo yeye ndiye anatokeza misiba ya asili; hilo linaonyesha kama hana huruma.”

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu.’ (1 Yohana 5:19) ‘Yule muovu’ ni nani? Biblia inaonyesha kama ni Shetani. (Mathayo 13:19; Marko 4:15) Je, jambo hilo ni kweli? Fikiria hili: Ikiwa Shetani anatawala ulimwengu, je, hauone kama ni yeye ndiye anachochea watu wawe wachoyo, wenye tamaa, na wenye kujifikiria kama yeye? Jambo hilo linatusaidia kuelewa sababu gani watu wanaharibu mazingira yao wenyewe duniani, sivyo? Watu wengi wenye elimu wanaonya kwamba kuharibu mazingira kunaweza kuchangia pia katika kutokeza misiba ya asili, kuifanya iwe mingi zaidi, ao yenye matokeo mabaya zaidi juu ya watu.

Kwa hiyo, sababu gani Mungu anamuacha Shetani awe na uvutano mwingi zaidi? Ili kupata jibu kwa ulizo hilo, inaomba kufikiria mambo yaliyotokea katika mwanzo wa historia ya wanadamu, wakati wazazi wetu wa kwanza waliasi utawala wa Mungu. Tangu wakati huo, watu wengi wamefuata mufano wao. Uamuzi huo wa kukataa utawala wa Mungu umeweka ulimwengu katika mikono ya Shetani, adui wa Mungu. Yesu alimuita Shetani ‘mutawala wa ulimwengu.’ (Yohana 14:30) Je, Shetani atatawala milele? Hapana!

Yehova * anahangaishwa kabisa na mateso ambayo Shetani anatokeza. Kwa kweli, Yehova anahuzunishwa sana watu wanapoteseka. Kwa mufano, kuhusu hali ngumu zilizofikia taifa la Israeli, Biblia inasema juu ya Mungu hivi: ‘Wakati wa taabu zao zote hilo lilimutaabisha.’ (Isaya 63:9) Kwa sababu ya huruma yake, Mungu amepanga kumaliza utawala wa Shetani hivi karibuni! Amemuweka Mwana wake Yesu Kristo kuwa Mufalme mwenye haki na muadilifu milele.

NAMNA GANI ULIZO HILO LINAKUHUSU WEWE: Hata kama utawala wa Shetani umeshindwa kulinda watu kutokana na misiba, utawala wa Yesu utafanya hivyo. Wakati fulani, Yesu aliwalinda wanafunzi wake kutokana na zoruba kali. Biblia inasema hivi: ‘Akaukemea upepo na kuiambia bahari: Nyamaza, utulie! Na upepo ukapunguka, kukawa utulivu mukubwa.’ Wanafunzi wakasema: ‘Kwa kweli huyu ni nani, kwa sababu hata upepo na bahari zinamutii?’ (Marko 4:37-41) Tukio hilo linatuhakikishia kama Yesu atawalinda watu wote watiifu wakati wa utawala wake.​—Danieli 7:13, 14.

^ Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.