Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Dunia Isiyokuwa na Chuki—Itakuwa Wakati Gani?

Dunia Isiyokuwa na Chuki—Itakuwa Wakati Gani?

“NINA ndoto.” Miaka 50 iliyopita, tarehe 28 Mwezi wa 8, mwaka wa 1963, Muamerika anayeitwa Martin Luther King, aliyekuwa muteteaji wa haki za raia, alisema maneno hayo katika hotuba yake yenye kujulikana sana. Kwa kutumia maneno hayo yenye kuvutia, King alieleza ndoto yake, ao tumaini lake kwamba siku moja watu wataishi bila kuchukia watu wengine kwa sababu ya rangi yao ya ngozi. Ijapokuwa maneno yake hayo yenye matumaini yalielekezwa kwa wasikilizaji wa huko Amerika, wazo kubwa la maneno hayo limekubaliwa na watu katika mataifa mengi.

Martin Luther King, akitoa hotuba yake juu ya haki za raia

Miezi mitatu kisha hotuba ya King, tarehe 20 Mwezi wa 11, 1963, inchi zaidi ya 100 zilikubali Azimio la Umoja wa Mataifa juu ya Kumaliza Aina Yoyote ya Ubaguzi wa Rangi. Makubaliano mengine yaliyofanywa yalikubaliwa katika makumi ya miaka iliyofuata. Bila shaka, bidii hizo zote nzuri zinatokeza ulizo hili, Matokeo yamekuwa nini?

Tarehe 21 Mwezi wa 3, 2012, Ban Ki-moon, Katibu Mukubwa wa Umoja wa Mataifa alisema hivi: “Kuna makubaliano mengi mazuri ambayo yamefanywa na mipango ambayo imechukuliwa na pia mambo mengine ambayo yanafanyika katika dunia yote ili kuzuia na kumaliza ubaguzi, ubaguzi wa rangi, chuki ya kutokubali na kuvumilia wageni. Hata hivyo, ubaguzi unaendelea kutokeza mateso kwa mamilioni ya watu katika dunia yote.”

Hata katika inchi ambamo maendeleo fulani yamefanywa ili kokomesha ubaguzi na aina mbalimbali za chuki, bado ulizo hili linajitokeza: Je, maendeleo ambayo yamefanywa yameondoa kabisa mawazo ya chuki yaliyo ndani ya mioyo ya watu ao je, maendeleo hayo yamewafundisha watu kutoonyesha chuki yao kuelekea wengine? Watu fulani wanaamini kwamba maendeleo hayo yanasaidia tu kuzuia ubaguzi, lakini hayana nguvu za kukomesha kabisa chuki. Sababu gani? Kwa sababu ubaguzi ni tendo ambalo linaweza kuonekana na kuazibiwa na sheria, lakini chuki inahusiana na mawazo yaliyo ndani ya akili na mioyo ya watu, ambayo hayawezi kuzuiwa kwa urahisi.

Kwa hiyo, bidii yoyote ya kumaliza chuki haipaswe tu kuzuia matendo ya ubaguzi lakini inapaswa pia kubadilisha mawazo ya mutu na namna anavyojisikia kuelekea watu wa kikundi kingine. Je, hilo linawezekana kabisa? Ikiwa ndiyo, namna gani? Acheni tuone mifano fulani ya kweli ambayo itatusaidia kuona kwamba inawezekana watu wabadilike na kwamba kuna jambo fulani ambalo linaweza kuwasaidia kufanya hivyo.

BIBLIA ILIWASAIDIA KUSHINDA CHUKI

“Sasa ninajisikia kuwa nimefunguliwa kutokana na mutego wa chuki.”​—Linda

Linda: Nilizaliwa huko Afrika ya Kusini. Nilimuona kila mutu aliyezaliwa huko Afrika ya Kusini ambaye hakuwa muzungu kuwa mutu wa hali ya chini, asiye na elimu, asiyetumainika, na anayepaswa kuwatumikia wazungu. Nilinaswa na mutego wa chuki katika namna yangu ya kuwaza na sikutambua jambo hilo. Lakini mawazo hayo yalianza kubadilika nilipoanza kujifunza Biblia. Nilijifunza kwamba “Mungu hana ubaguzi” na kwamba moyo ni wa maana zaidi kuliko rangi ya ngozi yetu ao luga ambayo tunazungumuza. (Matendo 10:34, 35; Methali 17:3) Andiko la Wafilipi 2:3 lilinisaidia kuelewa kwamba ningeweza kushinda chuki ikiwa ninamuona kila mutu kuwa bora kuliko mimi. Kuishi kulingana na kanuni za Biblia kama hizo kulinisaidia kupendezwa na wengine bila kujali rangi ya ngozi yao. Sasa ninajisikia kuwa nimefunguliwa kutokana na mutego wa chuki.

“Nilifikia kujua namna Mungu anavyowaona watu.”​—Michael

Michael: Nilikomalia katika eneo ambamo mulikuwa wazungu wengi wa Australia, na nilikuwa na chuki kali kuelekea watu wa Asia, zaidi sana Wachina. Nilipokuwa nikitembeza motokari na kuona mutu fulani anayefanana kuwa wa asili ya Asia, nilikuwa ninafungua kioo cha motokari yangu na kumutukana kwa kusema maneno kama vile “Wewe mutu wa Asia, rudia kwenu!” Kisha, nilipoanza kujifunza Biblia, nilifikia kujua namna Mungu anavyowaona watu. Anawapenda bila kujali mahali wanatoka ao sura yao. Upendo huo wa Mungu uligusa moyo wangu, na chuki yangu ikageuka kuwa upendo. Mabadiliko hayo makubwa ni yenye kushangaza. Sasa ninafurahi sana kushirikiana na watu kutoka inchi zote na wa hali zote. Hilo limefungua mawazo yangu kuhusu maisha na limeniletea furaha nyingi.

“Nilibadilisha mawazo yangu na nikafanya amani.”​—Sandra

Sandra: Mama yangu alikuwa mutu wa muji wa Umunede katika Jimbo la Delta, huko Nigeria. Lakini, watu wa familia ya baba yangu walitoka katika Jimbo la Edo na walizungumuza luga ya Esan. Kwa sababu hiyo, mama yangu alichukiwa sana na watu wa familia ya baba yangu mupaka alipokufa. Kwa hiyo, niliapa kwamba siwezi kushirikiana hata kidogo na mutu yeyote anayezungumuza luga ya Esan na kwamba siwezi hata kuolewa na mutu yeyote wa Jimbo la Edo. Lakini nilipoanza kujifunza Biblia, nilianza kuona mambo kwa njia tofauti. Kwa sababu Biblia inasema kwamba Mungu hana ubaguzi na kwamba kila mutu anayemuogopa anakubaliwa naye, mimi ni nani ili kuchukia watu kwa sababu ya kabila ao luga yao? Nilibadilisha mawazo yangu na nikafanya amani pamoja na watu wa familia ya baba yangu. Kutumia kanuni za Biblia kumenisaidia kuwa na furaha na amani ya akili. Pia, kumenisaidia kuwa na uhusiano muzuri na watu wengine bila kujali hali yao, rangi ya ngozi yao, luga yao, ao taifa lao. Na munajua niliolewa na mwanaume wa wapi? Mwanaume wa Jimbo la Edo anayezungumuza luga ya Esan.

Sababu gani Biblia imeweza kusaidia watu hao na wengine wengi kushinda chuki yao kali na ubaguzi? Ni kwa sababu Biblia ni Neno la Mungu. Ina nguvu ya kubadilisha namna mutu anavyofikiri na kujisikia kuhusu watu wengine. Zaidi ya hilo, Biblia inaonyesha jambo lingine linalohitajiwa ili kumaliza chuki yote.

UFALME WA MUNGU UTAMALIZA CHUKI YOTE

Hata ikiwa ujuzi wa Biblia unaweza kusaidia watu kuzuia na kumaliza chuki kali, kuna mambo mengine mawili yanayopaswa kushugulikiwa mbele ya kumaliza chuki kabisa. Jambo la kwanza, kuna zambi na kutokamilika kwa wanadamu. Biblia inasema waziwazi hivi: ‘Hakuna mwanadamu asiyetenda zambi.’ (1 Wafalme 8:46) Kwa hiyo, hata tujikaze namna gani, sisi pia tuna pambano la ndani kama mutume Paulo, aliyeandika hivi: “Ninapotaka kufanya yaliyo sawa, yaliyo mabaya yapo pamoja nami.” (Waroma 7:21) Ndiyo sababu, mara kwa mara, moyo wetu usio mukamilifu utakuwa na “mawazo mabaya” yanayoweza kutufanya tuwe na chuki.​—Marko 7:21.

Jambo la pili, Shetani Ibilisi anachochea watu kuwa na chuki. Biblia inasema kama yeye ni “muuaji” na kwamba ‘anaipotosha dunia nzima inayokaliwa.’ (Yohana 8:44; Ufunuo 12:9) Hilo linaonyesha sababu gani chuki inaenea sana na sababu gani wanadamu wanashindwa kuondoa chuki, ubaguzi, mauaji ya watu wengi, na aina nyingine ya kutovumilia watu wengine kwa sababu ya rangi yao ya ngozi, dini, na jamii yao.

Kwa hiyo, mbele ya kumaliza kabisa chuki, zambi na kutokamilika kwa wanadamu na uvutano wa Shetani vinapaswa kuondolewa kwanza. Biblia inaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu utaondoa mambo hayo.

Yesu Kristo alifundisha wanafunzi wake wasali hivi: “Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:10) Ufalme wa Mungu ni njia ambayo Mungu atatumia ili kumaliza ukosefu wote wa haki kutia ndani aina zote za kutovumilia watu wengine na chuki.

Wakati Ufalme wa Mungu utakuja kuongoza mambo hapa duniani, Shetani ‘atafungwa’ ao kuzuiwa kabisa ili “asipotoshe mataifa” tena. (Ufunuo 20:2, 3) Ndipo kutakuwa ‘dunia mupya’ ao jamii mupya ya wanadamu ambamo “uadilifu [ao haki] utakaa.” *​—2 Petro 3:13.

Wale watakaoishi katika jamii hiyo ya wanadamu yenye haki watafanywa kuwa wakamilifu, watu wasiofanya zambi. (Waroma 8:21) Kwa sababu watakuwa raia wa Ufalme wa Mungu, ‘hawatasababisha mazara yoyote wala kusababisha uharibifu wowote.’ Kwa nini? ‘Kwa maana dunia hakika itajawa na kumujua Yehova.’ (Isaya 11:9) Wakati huo, wanadamu wote watajifunza njia za Yehova Mungu na kuiga sifa zake nzuri. Bila shaka, hilo litamaanisha mwisho wa chuki yote, “kwa maana hakuna ubaguzi kwa Mungu.”​—Waroma 2:11.

^ Ili kupata habari zingine kuhusu Ufalme wa Mungu na mambo ambayo utafanya hivi karibuni, soma sura ya 3, ya 8, na ya 9 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.