Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mwisho wa Mateso Unakaribia!

Mwisho wa Mateso Unakaribia!

Wazia unaishi katika dunia isiyokuwa na mateso, dunia ambamo hakuna uvunjaji wa sheria, vita, magonjwa, na misiba ya asili. Wazia unaamuka kila asubuhi bila wasiwasi juu ya ubaguzi, uonevu, ao matatizo ya kifeza. Je, unafikiri ni ndoto tu kuamini kwamba mateso hayo yote yataisha? Ni kweli kwamba hakuna mwanadamu wala shirika lolote la wanadamu linaloweza kuleta mabadiliko kama hayo duniani. Lakini Mungu ameahidi kumaliza sababu zote zinazowaletea wanadamu mateso, kutia ndani sababu ambazo tulizungumuzia katika habari iliyotangulia. Ona ahadi zinazofuata ambazo zinatoka katika Neno la Mungu, Biblia:

‘Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mupaka wakati usio na kipimo.’​—Danieli 2:44.

Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni. Yesu Kristo, aliyechaguliwa ili kuwa Mutawala wa serikali hiyo, atachukua nafasi ya watawala wa kibinadamu na atahakikisha kwamba mapenzi ya Mungu yanafanywa duniani kama yanavyofanywa mbinguni. (Mathayo 6:9, 10) Hakuna serikali yoyote ya wanadamu ambayo itachukua nafasi ya serikali hiyo kwa sababu ni “ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.” Kutakuwa na amani isiyo na mwisho.​—2 Petro 1:11.

‘Shetani mwenyewe anaendelea kujigeuza mwenyewe kuwa malaika wa nuru. Kwa hiyo si jambo kubwa kama wahudumu wake wakiendelea pia kujigeuza wenyewe kuwa wahudumu wa uadilifu. Lakini mwisho wao utakuwa kulingana na matendo yao.’​—2 Wakorintho 11:14, 15.

Dini ya uongo itaonyeshwa wazi kuwa kazi ya Ibilisi na itaondolewa duniani. Hakutakuwa tena ubaguzi na umwangaji wa damu unaochochewa na dini. Hilo litawawezesha wale wote wanaomupenda “Mungu aliye hai na wa kweli” wamuabudu katika “imani moja” na “kwa roho na kweli.” Hilo litafanya kuwe amani na umoja kabisa!​—1 Wathesalonike 1:9; Waefeso 4:5; Yohana 4:23.

“Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”​—Ufunuo 21:3, 4.

Yehova Mungu atawezesha jambo hilo kupitia Mwana wake, Yesu, aliyetoa uzima wake kwa ajili ya wanadamu. (Yohana 3:16) Chini ya uongozi wa Yesu, wanadamu watafanywa kuwa wakamilifu. Hakutakuwa tena mateso yoyote kwa sababu “Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao” na atafuta “kila chozi kutoka katika macho yao.” Kutokamilika kwa wanadamu na mateso litakuwa jambo la wakati uliopita; “waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.”​—Zaburi 37:29.

‘Naye [Yesu Kristo] akamukamata yule joka mukubwa, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, na kumufunga kwa miaka elfu. Naye akamutupa ndani ya abiso na kuifunga na kuitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena.’​—Ufunuo 20:2, 3.

Uchochezi wote wa Shetani utaisha wakati Shetani na mashetani wake watafungwa na kutupwa ndani ya “abiso,” ni kusema, hali ya kutotenda kabisa. Hawatawachochea tena watu ili kutenda mambo mabaya. Litakuwa jambo lenye kutuliza kabisa kuishi katika dunia isiyokuwa na uchochezi wa Shetani na mashetani wake!

“Siku za mwisho” zitafikia mwisho wake mwishoni mwa kipindi ambacho Yesu aliita ‘ziki kubwa.’ Alisema hivi: ‘Ndipo kutakapokuwa na ziki kubwa ya namna ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mupaka sasa, hapana, wala haitatukia tena.’​—Mathayo 24:21.

Ziki hiyo itakuwa kubwa katika maana ya kwamba kutakuwa mateso ambayo hayajapata kutokea kabisa. Mateso hayo yatafikia mwisho wake kwenye “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote,” inayoitwa “Har-magedoni.”​—Ufunuo 16:14, 16..

Watu wa kila mahali wanaopenda mambo yaliyo sawa wanangojea kwa hamu mwisho wa ulimwengu huu muovu. Fikiria tu baraka chache ambazo wanangojea kupata wakati wa utawala wa Ufalme wa Mungu.

MUNGU ATAFANYA MAMBO MENGI ZAIDI!

‘Umati [ao mukutano] mukubwa’ utaokolewa na kuingia katika dunia mupya yenye amani: Neno la Mungu linasema kwamba ‘umati mukubwa’ wa watu ambao hawawezi kuhesabika wataokoka ‘kutoka ile ziki kubwa’ na kuingia katika dunia mupya yenye haki. (Ufunuo 7:9, 10, 14; 2 Petro 3:13) Watasema kwamba wokovu wao unatokana na Yesu Kristo, ‘Mwana-Kondoo wa Mungu ambaye anaondolea mbali zambi ya ulimwengu.’​—Yohana 1:29.

Mafundisho ya Mungu yataleta faida nyingi: Katika dunia mupya, ‘dunia hakika itajawa na kumujua Yehova.’ (Isaya 11:9) Mafundisho hayo ya Mungu yatatia ndani maagizo kuhusu namna ya kuishi kwa amani pamoja na watu wote na namna ya kutunza mazingira. Mungu anaahidi hivi: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.”​—Isaya 48:17.

Watu ambao tunawapenda waliokufa watafufuliwa kutoka katika makaburi: Wakati Yesu alikuwa hapa duniani, alimufufua rafiki yake Lazaro. (Yohana 11:1, 5, 38-44) Kwa kufanya hivyo, alionyesha namna atafufua watu wengi zaidi wakati wa utawala wa Ufalme wa Mungu.​—Yohana 5:28, 29.

Kutakuwa amani na haki milele: Wakati wa utawala wa Kristo, matendo ya uasi-sheria hayatakuwa tena. Namna gani tunajua jambo hilo? Kwa sababu Yesu ana uwezo wa kusoma mioyo, na atatumia uwezo wake kuhukumu kati ya wenye haki na waovu. Wale ambao wanakataa kubadili njia zao mbaya hawataruhusiwa kuishi katika dunia mupya ya Mungu.​—Zaburi 37:9, 10; Isaya 11:3, 4; 65:20; Mathayo 9:4.

Tumechunguza unabii mudogo tu kati ya unabii mwingi wa Biblia ambao unaonyesha mambo mazuri ya wakati unaokuja. Wakati Ufalme wa Mungu utatawala dunia yote, kutakuwa “wingi wa amani” milele. (Zaburi 37:11, 29) Mambo yote yanayofanya kuwe maumivu na mateso ambayo yamewapata wanadamu hayatakuwa tena. Tunaweza kuwa na uhakika na jambo hilo kwa sababu Mungu anaahidi hivi: “Tazama! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya. . . . Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.”​—Ufunuo 21:5.

[Kwenye Picha Ilitoka]

© Silke Woweries/Corbis