Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA SABABU GANI KUNA MATESO MENGI SANA? YATAISHA WAKATI GANI?

Watu Wengi Sana Wasiokuwa na Kosa Wanauawa!

Watu Wengi Sana Wasiokuwa na Kosa Wanauawa!

Mutoto mudogo mwanamuke anayeitwa Noelle alikuwa muchangamufu na alipenda kuchora. Siku moja mangaribi katika majira ya joto, alikuwa akitembea-tembea katika uwanja na akatumbukia ndani ya kisima cha familia cha kuogelea. Alikufa majuma mawili mbele ya kusherehekea mwaka wa ine wa siku ya kuzaliwa kwake.

Charlotte, Daniel, Olivia, Josephine . . . Hayo ni majina ya vijana fulani kati ya vijana 26 waliokuwa na miaka 26 ao 27 ambao walipigwa risasi kwenye masomo huko Connecticut, Amerika, tarehe 14 Mwezi wa 12, 2012. Kwenye maziko ya vijana hao, Raisi Obama aliita majina yao na akawaambia watu waliokuwa wakiomboleza hivi: “Matukio haya yenye kuhuzunisha sana yanapaswa kuisha.”

Bano aliyekuwa na miaka 18, alitoka Iraki mwaka wa 1996 na kuhamia Norwe (Norvège) pamoja na familia yake. Marafiki wake walimuita kwa jina la utani Sun Rays. Hata hivyo, jambo la kuhuzunisha ni kwamba tarehe 22 Mwezi wa 7, 2011, Bano alikuwa mumoja kati ya watu 77 ambao waliuawa na mutu mwenye imani kali ya kidini. Mutu huyo alisema hivi kwa kujisifu: “Ninaomba musamaha . . . kwamba sikuweza kuua watu wengi zaidi.”

Habari kama hizo zenye kuhuzunisha sana zimetangazwa tena na tena duniani pote. Fikiria huzuni na uchungu ambao unatokana na aksidenti, uvunjaji wa sheria, vita, ugaidi, misiba ya asili, na matukio mengine yenye kuhuzunisha sana. Watu wengi sana wasiokuwa na kosa wanauawa na wengine wengi sana wanateseka, mara nyingi bila sababu!

Watu fulani wanamulaumu Mungu, wakiwaza kwamba Muumbaji wetu hawahangaikie wanadamu. Wengine wanasema kwamba Mungu anaona mateso yetu lakini anaamua tu kutofanya jambo lolote. Lakini wengine wanasema kwamba matukio kama hayo yenye kuhuzunisha sana yamepangwa mbele ya wakati. Watu wana maoni mengi sana juu ya mateso yanayotupata. Ni wapi ambapo tunaweza kupata majibu yenye kutegemeka na yenye kutosheleza? Katika habari zinazofuata, tutachunguza katika Neno la Mungu, Biblia, ili kupata majibu kuhusu sababu zinazofanya watu wateseke na namna mateso yatakavyomalizwa.