Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Unaweza kufanya nini ili ndoa yako iwe yenye furaha?

Shauri la Biblia juu ya kufanya ndoa iwe yenye furaha lina matokeo mazuri kwa sababu linatoka kwa Yule aliyeanzisha ndoa, Yehova Mungu. Biblia inatufundisha tukomalishe sifa ambazo zinaweza kufanya ndoa yetu iwe yenye furaha na inatuonya juu ya tabia ambazo zinaweza kuharibu ndoa. Pia inatufundisha ufundi wa kupashana habari ambao unaongeza furaha katika ndoa.​—Soma Wakolosai 3:8-10, 12-14.

Bwana na bibi wanapaswa kuheshimiana. Ikiwa wote wawili wanakubali madaraka ambayo Mungu amewapatia katika ndoa, wanaweza kuwa wenye furaha.​—Soma Wakolosai 3:18, 19.

Ni nini kinachofanya ndoa idumu?

Bibi na bwana waliooana wanaweza kuendelea kukaa pamoja ikiwa wanapendana. Mungu anatufundisha namna ya kupendana. Mungu na Mwana wake, Yesu, ni mifano mizuri ya upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine.​—Soma 1 Yohana 4:7, 8, 19

Ikiwa bibi na bwana wanaheshimu ndoa kwa kuiona kuwa mupango wa Mungu, wanaweza kuendelea kukaa pamoja. Mungu aliumba ndoa uwe muungano wenye kudumu kati ya mwanaume na mwanamuke ili familia ziwe na usalama. Ndoa inaweza kudumu kwa sababu Mungu aliumba wanaume na wanawake ili wasaidiane kwa kutimiziana mahitaji ya kimwili na ya moyoni. Pia aliwaumba kwa mufano wake, wakiwa na uwezo wa kuiga upendo wake.​—Soma Mwanzo 1:27; 2:18, 24.