Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wale watakaookoka siku za mwisho wataishi katika dunia paradiso

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Je, tunaishi katika “siku za mwisho”?

Ungejibuje?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Labda

Biblia inasema hivi

“Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1) Unabii wa Biblia na matukio tunayoona sasa, yanathibitisha kwamba hizi ni “siku za mwisho.”

Mambo mengine tunayojifunza katika Biblia

  • Vita, njaa, matetemeko, na magonjwa hatari ya kuambukiza, ni mambo yanayothibitisha kwamba hizi ni siku za mwisho.—Mathayo 24:3, 7; Luka 21:11.

  • Katika siku hizi za mwisho, jamii ya wanadamu imekumbwa na hali mbaya ya kiadili na watu hawajali uhusiano wao na Mungu.—2 Timotheo 3:2-5.

Wakati ujao wa wanadamu utakuwaje?

Baadhi ya watu huamini kwamba . . .Siku za mwisho zitakoma dunia na kila mtu atakapoharibiwa, ilhali wengine wanaamini kwamba hali zitaboreka. Wewe una maoni gani?

Biblia inasema

“Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.”Zaburi 37:29.

Ni nini kingine tunachojifunza katika Biblia?