Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 HABARI KUU | VITA VILIVYOUBADILI ULIMWENGU

Msababishaji Mkuu wa Vita na Kuteseka

Msababishaji Mkuu wa Vita na Kuteseka

Vita vya Kwanza vya Ulimwengu viliisha Novemba 11, 1918. Biashara zilifungwa, na watu wakashangilia kwa vifijo na nderemo barabarani. Lakini shangwe hiyo haikudumu. Tisho lingine hatari zaidi kuliko bunduki lilifuata punde tu baada ya vita vya ulimwengu.

Mnamo Juni 1918, wanajeshi waliokuwa vitani huko Ufaransa waliambukizwa ugonjwa wenye kuua unaojulikana kama homa ya Hispania. Punde si punde, homa hiyo ilithibitika kuwa hatari sana. Kwa mfano, kwa miezi michache tu iliua wanajeshi wengi wa Marekani nchini Ufaransa kuliko wale waliouawa vitani. Baada ya vita wanajeshi waliokuwa wameambukizwa walirudi makwao na hivyo kueneza ugonjwa huo haraka ulimwenguni pote.

Miaka iliyofuata baada ya vita ilikuwa na njaa na hali mbaya ya kiuchumi. Watu wengi barani Ulaya hawakuwa na chakula vita vilipokoma katika mwaka wa 1918. Kufikia mwaka wa 1923, pesa za Ujerumani hazikuwa na thamani yoyote. Miaka sita baadaye, uchumi ulimwenguni pote uliporomoka. Mwishowe, mwaka wa 1939, Vita vya Pili vya Ulimwengu vikaanza,—na kwa njia fulani vilikuwa mwendelezo wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu. Ni nini kilichokuwa kikisababisha misiba hiyo iliyofuatana?

ISHARA YA SIKU ZA MWISHO

Unabii wa Biblia unatusaidia kujua kilichosababisha matukio fulani ya kihistoria, na hasa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu. Yesu Kristo alitabiri wakati  ambapo ‘taifa lingesimama kupigana na taifa’ na kungekuwa na upungufu wa chakula na tauni duniani kote. (Mathayo 24:3, 7; Luka 21:10, 11) Aliwaambia wanafunzi wake kwamba misiba hiyo ingekuwa sehemu ya ishara ya siku za mwisho. Habari zaidi zinapatikana katika kitabu cha Ufunuo, ambacho kinaonyesha kwamba matatizo yaliyo duniani yalisababishwa na vita vilivyotokea mbinguni.—Ona sanduku “Vita Duniani na Vita Mbinguni.”

Kitabu hicho pia kinataja wapanda-farasi wanne. Wapanda-farasi watatu wanafananisha misiba ileile ambayo Yesu alikuwa ametabiri, yaani, vita, njaa, na tauni. (—Ona sanduku “Je, Kweli Wale Wapanda-Farasi Wanne Wako Mwendoni?”) Ni wazi kwamba vita vya kwanza vya ulimwengu vilianzisha matatizo ambayo bado yanaendelea mpaka leo. Biblia inafunua kwamba Shetani ndiye aliyeianzisha. (1 Yohana 5:19) Je, kuna yeyote anayeweza kumzuia?

Kitabu cha Ufunuo pia kinatuhakikishia kwamba Shetani ana “kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12) Hiyo ndiyo sababu amejawa na hasira na anachochea uovu usio na kifani hapa duniani. Hata hivyo, matatizo tunayoona yanathibitisha kwamba muda wake unakaribia kwisha.

 KUZIVUNJA KAZI ZA IBILISI

Kwa kweli Vita vya Kwanza vya Ulimwengu vilileta mabadiliko makubwa katika historia. Vilileta kipindi cha vita chenye maasi na kufanya watu wasiwaamini watawala. Pia, ni uthibitisho ulio wazi kwamba Shetani alikuwa amefukuzwa mbinguni. (Ufunuo 12:9) Mtawala huyo wa ulimwengu asiyeonekana alitenda kama dikteta mkatili ambaye anajua siku zake zimehesabiwa. Siku zake zitakwisha, matatizo ambayo yalisababishwa na Vita vya Kwanza vya Ulimwengu yatakoma.

Baada ya kuchunguza unabii wa Biblia, una sababu ya kuamini kwamba hivi karibuni Yesu Kristo, Mfalme wetu aliye mbinguni, ‘atazivunja kazi za Ibilisi.’ (1 Yohana 3:8) Tayari mamilioni ya watu wanasali Ufalme wa Mungu uje. Je, wewe husali hivyo? Kupitia Ufalme huo, watu waaminifu wataona mapenzi ya Mungu, bali si ya Shetani, yakitendeka duniani. (Mathayo 6:9, 10) Chini ya Ufalme wa Mungu, hakutakuwa tena na vita vya ulimwengu au vita vyovyote vile! (Zaburi 46:9) Jifunze kuhusu Ufalme huo ili uishi wakati ambapo kutakuwa na amani duniani!—Isaya 9:6, 7.

^ fu. 20 Ona sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.