Zaburi 46:1-11

  • “Mungu ni kimbilio letu”

    • Kazi za Mungu zinazostaajabisha (8)

    • Mungu akomesha vita katika dunia yote (9)

Kwa kiongozi. Wa wana wa Kora.+ Kulingana na mtindo wa Alamothi.* Wimbo. 46  Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu,+Msaada unaopatikana kwa urahisi nyakati za taabu.+   Ndiyo sababu hatutaogopa, hata dunia ikibadilika,Hata milima ikianguka katika vilindi vya bahari,+   Hata maji yake yakinguruma na povu lake kufurika,+Hata milima ikitikiswa na msukosuko wake. (Sela)   Kuna mto ambao vijito vyake hufanya jiji la Mungu lishangilie,+Hema la ibada la Aliye Juu Zaidi lililo takatifu na tukufu.   Mungu yuko katika jiji hilo;+ haliwezi kupinduliwa. Mungu atalisaidia wakati wa mapambazuko.+   Mataifa yalikuwa katika msukosuko, falme zilipinduliwa;Alipaza sauti yake, dunia ikayeyuka.+   Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.* (Sela)   Njooni mtazame matendo ya Yehova,Jinsi alivyotenda mambo yanayostaajabisha duniani.   Anakomesha vita katika dunia yote.+ Anauvunja upinde na kuuvunja mkuki vipandevipande;Anayateketeza magari ya vita motoni.* 10  “Salimuni amri na mjue kwamba mimi ni Mungu. Nitakwezwa miongoni mwa mataifa;+Nitakwezwa duniani.”+ 11  Yehova wa majeshi yuko pamoja nasi;+Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu salama.+ (Sela)

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “kilele chetu salama.”
Au labda, “Anaziteketeza ngao motoni.”