Kulingana na Mathayo 4:1-25

  • Ibilisi amjaribu Yesu (1-11)

  • Yesu aanza kuhubiri Galilaya (12-17)

  • Wanafunzi wa kwanza wachaguliwa (18-22)

  • Yesu ahubiri, afundisha, na kuponya (23-25)

4  Ndipo Yesu akaongozwa na roho kuingia nyikani ili akajaribiwe+ na Ibilisi.+  Baada ya kufunga kwa siku 40, mchana na usiku, akahisi njaa.  Naye Mjaribu+ akaja na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, yaambie mawe haya yawe mikate.”  Lakini akajibu: “Imeandikwa: ‘Mwanadamu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’”*+  Ndipo Ibilisi akampeleka kwenye lile jiji takatifu,+ akamsimamisha juu ya mnara* wa hekalu+  na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, jitupe chini, kwa maana imeandikwa: ‘Atawaagiza malaika zake kukuhusu wewe,’ nao ‘Watakubeba mikononi mwao, ili mguu wako usigonge jiwe.’”+  Yesu akamwambia: “Tena imeandikwa: ‘Usimjaribu Yehova* Mungu wako.’”+  Tena Ibilisi akampeleka Yesu kwenye mlima mrefu sana, akamwonyesha falme zote za ulimwengu na utukufu wazo.+  Naye akamwambia: “Nitakupa vitu hivi vyote ukianguka chini na kunifanyia tendo la ibada.” 10  Ndipo Yesu akamwambia: “Nenda zako, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Yehova* Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu,+ na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’”+ 11  Ndipo Ibilisi akamwacha,+ na tazama! malaika wakaja na kuanza kumhudumia.+ 12  Yesu aliposikia kwamba Yohana alikuwa amekamatwa,+ akaenda Galilaya.+ 13  Isitoshe, baada ya kuondoka Nazareti, akaenda kukaa Kapernaumu+ kando ya bahari katika wilaya za Zabuloni na Naftali, 14  ili kutimiza maneno haya yaliyosemwa kupitia nabii Isaya, aliyesema: 15  “Ewe nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kando ya barabara ya bahari, ng’ambo ya Yordani, katika Galilaya ya mataifa! 16  Watu wanaokaa katika giza waliona nuru kuu, na wale wanaokaa katika eneo la kivuli cha kifo, nuru+ iliwaangazia.”+ 17  Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri na kusema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”+ 18  Alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya aliwaona ndugu wawili, Simoni, anayeitwa Petro,+ na Andrea ndugu yake, wakishusha wavu baharini, kwa maana walikuwa wavuvi.+ 19  Akawaambia: “Nifuateni, nami nitawafanya muwe wavuvi wa watu.”+ 20  Mara moja wakaziacha nyavu zao na kumfuata.+ 21  Alipoenda mbele kidogo akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo.+ Walikuwa kwenye mashua pamoja na baba yao Zebedayo wakitengeneza nyavu zao, naye akawaita.+ 22  Mara moja wakaacha ile mashua na baba yao, wakamfuata. 23  Kisha akaenda katika Galilaya yote,+ akifundisha katika masinagogi+ yao na kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuwaponya watu kila aina ya ugonjwa na kila aina ya udhaifu.+ 24  Na habari kumhusu zikaenea katika Siria yote, nao wakamletea wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na walioteseka,+ wenye roho waovu+ na wenye kifafa+ na watu waliopooza, naye akawaponya. 25  Kwa hiyo, umati mkubwa ukamfuata kutoka Galilaya, Dekapoli,* Yerusalemu, Yudea, na ng’ambo ya Yordani.

Maelezo ya Chini

Au “ukuta wa ukingoni; sehemu ya juu zaidi.”
Au “Eneo lenye Majiji Kumi.”