Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maisha ya Familia na Urafiki

Maisha ya Familia na Urafiki

Watu mingi wanaona kama ni nguvu kuchunga urafiki wao pamoja na watu wa familia na marafiki. Ona kanuni fulani za Biblia zenye zinaweza kukusaidia kufanya urafiki wako pamoja na wengine ukuwe muzuri zaidi.

EPUKA UCHOYO

KANUNI YA BIBLIA: “Mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.”​—Wafilipi 2:4.

ILE INAMAANISHA NINI? Urafiki wa kweli unatokana na kutoa kuliko tu kupokea. Kama uko muchoyo, unaweza kuharibu urafiki wako pamoja na wengine. Kwa mufano, kama bibi ao bwana ni muchoyo, anaweza kufikia kukosa kuwa mwaminifu kwa mwenzake. Tena, hakuna mutu mwenye anapendaka kufanya urafiki na mutu mwenye iko na tabia ya kujisifu juu ya mambo yenye iko nayo ao yenye anajua. Kitabu The Road to Character kinasema kama, “watu wenye wanajifikiria wao wenyewe kuliko kufikiria watu wengine, wanapatwa na matatizo mingi.”

KILE UNAWEZA KUFANYA:

  • Usaidie wengine. Marafiki wa kweli wanatumainiana, na sikuzote wako tayari kusaidiana. Uchunguzi fulani unaonyesha kama watu wenye kusaidia wengine hawapatwe sana na ugonjwa wa kushuka moyo. Tena wanajisikia kuwa ni wa maana wakati wanafanya vile.

  • Ujitie pa nafasi ya wengine. Kujitia pa nafasi ya wengine ni uwezo wa kujisikia namna wengine wanajisikia wakati wako mu magumu. Kama unajitia pa nafasi ya wengine, bila shaka itakuwa nguvu kwako kutumia maneno yenye inaonekana kuwa ni mizaha lakini iko na kusudi la kuumiza mutu mwingine ao kumushushia heshima.

    Pia, wakati unajitia pa nafasi ya wengine, unakuwa tayari kuwavumilia. Kwa hiyo, kujitia pa nafasi ya wengine kunaweza kukusaidia uepuke ubaguzi na kukusaidia ukuwe na marafiki kutoka mu desturi ao mahali mbalimbali.

  • Pitisha wakati pamoja na wengine. Kadiri unapitisha wakati pamoja na watu wengine, ni vile unawajua muzuri zaidi. Unapaswa kuwa na mazungumuzo ya muzuri pamoja na wengine ili upate marafiki wa kweli. Kwa hiyo, ukuwe musikilizaji muzuri. Onyesha kuwa unahangaikia marafiki wako. Uchunguzi wa hivi karibuni unasema kama “mazungumuzo ya muzuri inaweza kufanya watu wakuwe na furaha zaidi.”

UCHAGUE MARAFIKI KWA HEKIMA

KANUNI YA BIBLIA: “Mashirika ya mubaya yanaharibu tabia za muzuri.”​—1 Wakorinto 15:33.

ILE INAMAANISHA NINI? Watu wenye unapitisha wakati pamoja nao, wanaweza kukuchochea kufanya mambo ya muzuri ao ya mubaya. Watu wenye wanajifunza tabia za watu wanasema kama rafiki anaweza kukuchochea mu hali mingi za maisha yako. Kwa mufano, wanasema kama ikiwa unazungukwa na watu wenye kuvuta tumbaku ao wenye wanapenda kuvunja ndoa, unaweza kufikia kuvuta ao kutaka kuvunja ndoa.

KILE UNAWEZA KUFANYA: Ufanye urafiki pamoja na watu wenye wako na sifa na kanuni za mwenendo zenye unapenda ao wenye ungependa kuiga. Kwa mufano, upitishe wakati pamoja na watu wenye kuwa na sifa kama vile adabu, heshima, ukarimu, na ukaribishaji-wageni.

KANUNI ZINGINE ZA BIBLIA

Angalia video zenye kutegemea Biblia zenye zimetayarishwa ili kusaidia bibi na bwana, vijana, na watoto kufanya maisha yao ya familia ikuwe ya muzuri zaidi

EPUKA MANENO YENYE KUUMIZA.

“Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga.”​—MEZALI 12:18.

UKUWE MUKARIMU.

“Mutu mukarimu atafanikiwa.”​—MEZALI 11:25.

UTENDEE WENGINE NAMNA UNGEPENDA WAKUTENDEE.

“Mambo yote yenye munataka watu wawatendee, ninyi pia lazima muwatendee wao.”​—MATAYO 7:12.