Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo ya Feza

Mambo ya Feza

Watu mingi wako na matatizo kidogo ya feza kwa kutumikisha kanuni za Biblia.

UFANYE MIPANGO YA MUZURI

KANUNI YA BIBLIA: “Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio, lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.” ​—Mezali 21:5.

ILE INAMAANISHA NINI? Ili ufanikiwe mu maisha, ni jambo la lazima ushikamane sana na mipango yenye umefanya. Kwa hiyo, upange namna utatumia feza yako mbele ya kuuza kitu chochote. Kumbuka, pengine hautakuwa na feza ya kununua kila kitu chenye unapenda. Kwa hiyo, utumie feza zako kwa hekima.

KILE UNAWEZA KUFANYA:

  • Uheshimie namna umepanga kutumia feza zako. Fanya liste ya vitu vyote vyenye unapanga kuuza na uvipange kulingana na aina, kama vile chakula, nguo, na nyumba. Kisha upange feza zenye utatumia juu ya kila kitu. Kama unafikia kutumia feza mingi juu ya kununua kitu fulani, kamata feza kwa zile zenye ulipanga kutumia juu ya kitu kingine. Kwa mufano, kama ulitumia feza mingi ili kununua esanse, kamata kwa zile zenye ulipanga juu ya kununua kitu fulani chenye hakiko cha lazima sana​—kwa mufano, feza ya kutumia ku restora.

  • Epuka deni zenye haziko za lazima. Kama inawezekana, uepuke deni. Kuliko kukamata deni, ukuwe unaweka feza kidogo-kidogo ili kufikia kununua kitu chenye uko nacho lazima. Kama unalazimika kujikopesha feza, ujikaze kulipa mbele ya wakati juu deni isiongezeke. Kama uko na deni, ufanye mipango ya kulipa ile deni na uiheshimie.

    Mutu mwenye kuwa na tabia ya kujikopesha feza, anakuwaka pia na zoezi ya kuzitumia sana. Kwa hiyo, kama unaona ni lazima ujikopeshe, ufikiri sana mbele ya kufanya vile.

FANYA ANGALISHO NA TABIA ZA MUBAYA

KANUNI YA BIBLIA: “Muvivu halime wakati wa kipindi cha baridi, kwa hiyo atakuwa anaomba-omba katika kipindi cha mavuno wakati hatakuwa na kitu.”​—Mezali 20:4.

ILE INAMAANISHA NINI? Kuwa muvivu kunaweza kumufanya mutu akuwe maskini. Kwa hiyo, ukuwe mufanyakazi mwenye bidii, na ujikaze kutumia feza zako kwa hekima juu usikose kitu fulani chenye utakuwa nacho lazima wakati wenye kuja.

KILE UNAWEZA KUFANYA:

  • Utumike kwa bidii. Wakati uko mufanyakazi mwenye bidii na mwenye kutumainika, wakubwa wako wa kazi watakupenda na hawatapenda kukuacha.

  • Ukuwe muaminifu. Usiibe feza ao vitu vya mukubwa wako wa kazi. Kukosa uaminifu kunaweza kukuharibishia sifa na kufanya ikuwe nguvu kwa watu wengine kukupatia kazi.

  • Epuka kuwa na pupa. Kuwa na mawazo yenye haifae juu ya feza, kunaweza kufikia kuharibu afya yako na uhusiano wako pamoja na watu wengine. Kumbuka, feza haiko njo jambo la maana zaidi mu maisha.

KANUNI ZINGINE ZA BIBLIA

Soma Biblia ku site yetu ya Enternete jw.org. Inapatikana katika mamia ya luga

USIPOTEZE WAKATI NA FEZA KWA AJILI YA TABIA ZA MUBAYA.

“Mulevi na mulafi watakuwa maskini, na kusinzia kutavalisha mutu nguo zenye kupasuka-pasuka.”​—MEZALI 23:21.

EPUKA KUHANGAIKA SANA JUU YA FEZA.

“Muache kuhangaikia uzima wenu juu ya kile mutakula ao kile mutakunywa, ao miili yenu juu ya kile mutavaa.”​—MATAYO 6:25.

EPUKA WIVU.

“Mutu mwenye wivu anajikaza sana kupata mali, lakini hajue kwamba umaskini utamupata.”​—MEZALI 28:22.