Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Afya ya Moyoni

Afya ya Moyoni

Biblia inatuonya tuepuke tabia zenye kuwa hatari kwa afya na inatutia moyo kukomalisha tabia zenye zinatuletea faida.

KASIRANI

KANUNI YA BIBLIA: “Mutu mwenye hakasirike haraka ni muzuri zaidi kuliko mwanaume mwenye nguvu.”​—Mezali 16:32.

ILE INAMAANISHA NINI? Tunapata faida wakati tunafikia kuzuia hisia zetu. Hata kama wakati fulani tunaweza kuwa na sababu ya kukasirika, kukosa kuzuia kasirani yetu kunaweza kuleta matokeo ya mubaya sana. Utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kama wakati watu ni wenye kukasirika, hawafikiri muzuri na mara mingi wanafanya ao kusema mambo yenye itawafanya wafikie kuhuzunika.

KILE UNAWEZA KUFANYA: Ujifunze kuzuia kasirani yako mbele ikutawale. Watu fulani wanawaza kama kukosa kuzuia kasirani ni alama ya kuwa na nguvu, lakini kwa kweli, ile ni alama ya uzaifu. Biblia inasema: “Kama muji wenye umebomolewa, wenye hauna ukuta ni vile pia mutu mwenye hawezi kuzuia kasirani yake.” (Mezali 25:28) Njia moja ya muzuri ya kuzuia kasirani yako ni kuelewa mambo yote yenye ilifanyika mbele ya kutenda. “Ufahamu wa mutu hakika unatuliza kasirani yake.” (Mezali 19:11) Ni jambo la maana tuelewe muzuri mambo yenye ilifanyika mbele ya kutenda jambo fulani; ile inaweza kutusaidia kutulia.

KUWA MWENYE SHUKRANI

KANUNI YA BIBLIA: “Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.”​—Wakolosai 3:15.

ILE INAMAANISHA NINI? Inasemekana kama ni wale tu wenye kuwa na shukrani njo wanaweza kuwa na furaha. Hata wale wenye wamefiwa ao kupoteza kitu cha bei sana wanakubaliana na jambo hilo. Wanasema kama jambo lenye linawasaidia ni kukaza akili juu ya mambo yenye inawafanya wakuwe wenye shukrani, hapana kukaza akili juu ya mambo yenye wamepoteza.

KILE UNAWEZA KUFANYA: Kila siku, fanya liste ya vitu vyenye vinafanya ukuwe mwenye shukrani. Haiko lazima vikuwe vitu vikubwa. Fikiri hata juu ya vitu vidogo-vidogo, kama vile mwangaza wa jua wenye kupendeza wa asubui, mazungumuzo yenye kufurahisha pamoja na mutu mwenye unapenda, ao kwa sababu ya kupitisha siku fulani muzuri. Kama unakamata wakati wa kuifikiria na kuonyesha shukrani juu ya ile mambo, ile inaweza kufanya afya yako ya moyoni ikuwe muzuri zaidi.

Inaweza kuwa muzuri zaidi kama unafikiri juu ya jambo lenye linakufanya ukuwe mwenye shukrani kwa watu wa familia yako na marafiki. Wakati unatambua jambo lenye linakufanya ukuwe mwenye shukrani kwa watu wengine, uwaambie jambo hilo. Unaweza kufanya vile moja kwa moja ao kupitia barua, ao kwa kuwaandikia ujumbe. Bila shaka, ile itafanya urafiki wenu ukuwe wenye nguvu na utajionea furaha yenye inatokana na kutoa.​—Matendo 20:35.

KANUNI ZINGINE ZA BIBLIA

Unaweza kuchukua ku Enternete usomaji wa Biblia wenye kurekodiwa. Unapatikana kwenye jw.org mu luga 40 hivi

EPUKA MABISHANO.

“Kuanzisha vita ni kama kufungua mulango mukubwa wa mafuriko; mbele ugomvi uanze, ondoka.”​—MEZALI 17:14.

EPUKA KUHANGAIKA KUPITA KIASI JUU YA WAKATI WENYE KUJA.

“Musihangaike hata kidogo juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku iko na matatizo yake yenye yanaeneana na siku hiyo.”​—MATAYO 6:34.

USITENDE MARA MOJA KULINGANA NA VILE UNAJISIKIA, LAKINI UFIKIRI KWA UANGALIFU MBELE UTENDE.

“Uwezo wa kufikiri utakulinda, na utambuzi utakuchunga.”​—MEZALI 2:11.