Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MAWAZO YA BIBLIA

Sala

Sala

Je, kuna mutu ambaye anasikia sala zetu?

‘Ee musikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.’ —Zaburi 65:2.

MAWAZO YA WATU

Imesemekana kwamba sala “haivuke sehemu ya juu ya nyumba.” Zaidi sana watu ambao wanapambana na mateso wanaweza kuwa na muelekeo wa kushakia kwamba Mungu anasikia sala.

MAWAZO YA BIBLIA

Biblia inasema hivi: ‘Macho ya Yehova [Mungu] yako juu ya waadilifu, na masikio yake yanasikiliza dua yao; bali uso wa Yehova uko zidi ya wale wanaotenda mambo mabaya.’ (1 Petro 3:12) Ni wazi kwamba, Mungu anasikiliza sala. Lakini anasikiliza sala za wale ambao wanafuata mafundisho yake. Kuhusu namna Mungu alivyo tayari kutusikiliza wakati tunamuomba, andiko lingine linasema hivi: ‘Huu ndio uhakika ambao tunao kwake, kwamba, hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.’ (1 Yohana 5:14) Ni lazima wale wanaomuomba Mungu kwa uaminifu watambue ni sala za aina gani ndizo zinaweza kupatana na mapenzi ya Mungu.

 Tunapaswa kusali namna gani?

Munaposali, musiseme mambo yaleyale tena na tena.’—Mathayo 6:7.

MAWAZO YA WATU

Waamini wengi wa dini mbalimbali kama vile, wabuda, wakatoliki, wahindu, na waislamu, wamefundishwa kutumia shanga ili kutoa sala ambazo wamechunga akilini na kuhesabu sala ambazo wanatoa.

MAWAZO YA BIBLIA

Sala zinapaswa kutoka moyoni na kutolewa kwa moyo wote; hatupaswe kuziweka katika akilini na kuzirudilia rudilia. Biblia inatushauria hivi: ‘Munaposali, musiseme mambo yaleyale tena na tena, kama vile watu wa mataifa wanavyofanya, kwa maana wao wanawaza watasikiwa kwa kutumia maneno mengi. Kwa hiyo, musijifanye kama wao, kwa maana Mungu Baba yenu anajua ni vitu gani munavyohitaji hata kabla hamujamwomba.’—Mathayo 6:7, 8.

SABABU GANI NI LAZIMA KUFANYA HIVYO?

Wakati sala inatolewa kwa njia isiyokubaliwa na Mungu, mutoaji wa sala hiyo anaweza kuwa akipoteza wakati wake ao labda kumuumiza Mungu. Biblia inaonya kwamba sala zinazotolewa na watu ambao wanakataa kujitiisha kwa mapenzi ya Mungu ni “chukizo” kwake.—Methali 28:9.

Tunapaswa kumuomba nani?

Mutafuteni Yehova, wakati anapoweza kupatikana. Mwiteni akiwa bado yupo karibu.’—Isaya 55:6.

MAWAZO YA WATU

Waamini fulani wanamuomba Maria ao viumbe vingine kama vile malaika na watu ambao wanaheshimiwa sana na kuonwa kuwa “watakatifu.” Kati ya watu hao kuna “Mutakatifu” Anthony wa Padua, ambaye inasemekana kuwa anashugulikia “mahitaji ya kiroho na yale yasiyo ya kiroho,” na “Mutakatifu” Jude, ambaye anaonwa kuwa mutakatifu mukubwa wa “hali za hatari.” Watu wengi wanasali kwa “watakatifu” kama hao na kwa malaika wakitumaini kwamba watawasemea mbele ya Mungu.

MAWAZO YA BIBLIA

Waabudu wa kweli wanapaswa kusali kwa ‘Baba yetu aliye mbinguni.’ (Mathayo 6:9) Biblia inatushauria hivi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.’Wafilipi 4:6.