Barua ya Pili kwa Wakorintho 9:1-15

  • Wachochewa kutoa (1-15)

    • Mungu humpenda mtoaji mchangamfu (7)

9  Basi kuhusu huduma ambayo ni kwa ajili ya watakatifu,+ kwa kweli si lazima niwaandikie ninyi,  kwa maana ninajua utayari wenu ambao ninajisifia kwa Wamakedonia, kwamba Akaya imekuwa tayari kwa mwaka mmoja sasa, na bidii yenu imewachochea wengi kati yao.  Lakini ninawatuma akina ndugu, ili kujisifu kwetu juu yenu kusiwe bure kuhusiana na jambo hilo, na kwamba muwe tayari kwelikweli, kama nilivyosema mtakuwa.  La sivyo, Wamakedonia wakija pamoja nami na kukuta hamko tayari, sisi—nanyi pia—tutaona aibu kwa sababu ya uhakika wetu kwenu.  Basi niliona ni jambo muhimu kuwatia moyo akina ndugu watangulie kuja kwenu na kuitayarisha mapema zawadi yenu ya ukarimu iliyoahidiwa, ili iwe tayari kama zawadi ya ukarimu, bali si kama kitu cha kulazimishwa.  Lakini kuhusu hili, yeyote anayepanda kwa uhaba atavuna pia kwa uhaba, naye anayepanda kwa wingi atavuna pia kwa wingi.+  Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda* wala kwa kulazimishwa,+ kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.+  Isitoshe, Mungu anaweza kufanya fadhili zake zote zisizostahiliwa ziwe nyingi kuwaelekea, ili sikuzote muwe na vitu vya kuwatosheleza kabisa katika kila jambo, na pia muwe na vingi kwa ajili ya kila kazi njema.+  (Kama ilivyoandikwa: “Amegawa kwa wingi;* amewapa maskini. Uadilifu wake unadumu milele.”+ 10  Basi Yule ambaye humgawia mpandaji mbegu kwa wingi na mkate wa kula atawagawia na kuwazidishia ninyi mbegu ili mzipande naye ataongeza mavuno ya uadilifu wenu.) 11  Katika kila jambo mnatajirishwa kwa ajili ya kila namna ya ukarimu, ambao kupitia kwetu hufanya watu wamshukuru Mungu; 12  kwa kuwa huduma ya utumishi huu wa watu wote si kuandaa vizuri tu mahitaji ya watakatifu+ bali pia kuwe na utajiri wa shukrani nyingi kwa Mungu. 13  Kupitia uthibitisho wa huduma hii ya kutoa msaada, wanamtukuza Mungu kwa sababu mnajitiisha kwenye habari njema kumhusu Kristo, kama mlivyotangaza hadharani, na kwa sababu ninyi ni wakarimu katika mchango wenu kwao na kwa wote.+ 14  Na kupitia dua kwa ajili yenu, wanaonyesha upendo wao kwenu kwa sababu ya fadhili nyingi zisizostahiliwa za Mungu juu yenu. 15  Shukrani kwa Mungu kwa ajili ya zawadi yake ya bure isiyoelezeka.

Maelezo ya Chini

Au “bila kutaka.”
Au “kwa ukarimu.”