Barua ya Pili kwa Wathesalonike 1:1-12

  • Salamu (1, 2)

  • Imani ya Wathesalonike yazidi kukua (3-5)

  • Kisasi dhidi ya wasiotii (6-10)

  • Sala kwa ajili ya kutaniko (11, 12)

1  Paulo, Silvano,* na Timotheo,+ kwa kutaniko la Wathesalonike katika muungano na Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:  Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo.  Tuna wajibu wa kumshukuru Mungu sikuzote kwa sababu yenu, akina ndugu. Hilo linafaa kwa kuwa imani yenu inakua sana na upendo wa kila mmoja wenu unaongezeka kati yenu.+  Ndiyo maana tunajivunia ninyi+ kati ya makutaniko ya Mungu kwa sababu ya uvumilivu na imani yenu katika mateso yenu yote na taabu* mnayopata.*+  Huu ni uthibitisho wa hukumu ya uadilifu ya Mungu, inayowaongoza kuhesabiwa kuwa mnastahili Ufalme wa Mungu, ambao kwa kweli mnateseka kwa ajili yake.+  Hii inazingatia kwamba ni jambo la uadilifu kwa Mungu kuwalipa dhiki wale wanaowasababishia ninyi dhiki.+  Lakini ninyi mnaopata dhiki mtapata kitulizo pamoja nasi wakati wa ufunuo wa Bwana Yesu+ kutoka mbinguni akiwa pamoja na malaika wake wenye nguvu+  katika mwali wa moto, atakapoleta kisasi juu ya wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema kumhusu Bwana wetu Yesu.+  Watu hao watapata hukumu ya adhabu ya uharibifu wa milele+ kutoka mbele za Bwana na kutoka kwa utukufu wa nguvu zake, 10  wakati atakapokuja kutukuzwa kuhusiana na watakatifu wake na kustaajabiwa siku hiyo kati ya wote walioonyesha imani, kwa sababu ushahidi tuliotoa ulikubaliwa kwa imani kati yenu. 11  Kwa hiyo, tunasali sikuzote kwa ajili yenu, kwamba Mungu wetu awahesabu kuwa mnastahili mwito wake+ na kwa nguvu zake kufanya kikamili mambo yote yanayompendeza na kila kazi ya imani. 12  Ili jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe ndani yenu nanyi katika muungano naye, kulingana na fadhili zisizostahiliwa za Mungu wetu na za Bwana Yesu Kristo.

Maelezo ya Chini

Pia anaitwa Sila.
Au “dhiki.”
Au “mnayovumilia.”