Kwa Tito 2:1-15

  • Ushauri unaofaa kwa wazee na vijana (1-15)

    • Kataa matendo yasiyompendeza Mungu (12)

    • Bidii kwa ajili ya matendo mema (14)

2  Hata hivyo, wewe endelea kusema mambo yanayopatana na fundisho lenye manufaa.*+  Wanaume wenye umri mkubwa wanapaswa kuwa wenye kiasi katika mazoea, wanaochukua mambo kwa uzito, wenye utimamu wa akili, wenye imani yenye afya, wenye upendo, na wavumilivu.  Vilevile wanawake wenye umri mkubwa wanapaswa kuwa wenye tabia ya kumhofu Mungu, wasiwe wachongezi, wala wasiwe watumwa wa divai nyingi, wawe walimu wa yaliyo mema;  ili wawashauri * wanawake vijana wawapende waume zao, wawapende watoto wao,  wawe na utimamu wa akili, safi kiadili, wanaofanya kazi nyumbani,* wema, wanaojitiisha kwa waume zao,+ ili neno la Mungu lisitukanwe.  Vivyo hivyo, endelea kuwahimiza wanaume vijana wawe na utimamu wa akili,+  ukiwawekea mfano mzuri wa matendo mema katika mambo yote. Fundisha mambo safi* kwa uzito wote,+  ukitumia maneno yenye manufaa* yasiyoweza kulaumiwa,+ ili kuwaaibisha wale wanaopinga, wakiwa hawana jambo lolote baya* la kusema kutuhusu.+  Watumwa na wajinyenyekeze kwa mabwana wao katika mambo yote,+ wakijitahidi kuwapendeza, wasibishane nao, 10  wasiwe wakiwaibia,+ bali wawe waaminifu kabisa, ili katika mambo yote walipambe fundisho la Mwokozi wetu, Mungu.+ 11  Kwa maana Mungu ameonyesha fadhili zisizostahiliwa kwa kuwaletea wokovu watu wa namna zote.+ 12  Nazo zinatuzoeza kukataa matendo yasiyompendeza Mungu na tamaa za ulimwengu+ na kuishi kwa utimamu wa akili, uadilifu, na ujitoaji-kimungu* katika mfumo huu wa mambo,*+ 13  huku tukingojea tumaini lenye furaha+ na kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu mkuu na kwa Mwokozi wetu, Yesu Kristo, 14  aliyejitoa kwa ajili yetu+ ili atuweke huru*+ kutoka katika kila namna ya uasi sheria na kujisafishia watu walio mali yake ya pekee, wenye bidii katika matendo mema.+ 15  Endelea kusema mambo haya na kuhimiza* na kukaripia kwa mamlaka kamili.+ Usiache mtu yeyote akudharau.

Maelezo ya Chini

Au “lenye afya; lenye faida.”
Au “wawakumbushe; wawazoeze.”
Au “wanaotunza nyumba zao.”
Au labda, “Fundisha kwa usafi.”
Au “yenye afya; yenye faida.”
Au “ovu.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Tnn., “atutolee fidia; atukomboe.”
Au “kutia moyo.”