Kwa Waroma 12:1-21

  • Toeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai (1, 2)

  • Zawadi mbalimbali lakini mwili mmoja (3-8)

  • Ushauri kuhusu maisha ya Wakristo wa kweli (9-21)

12  Kwa hiyo akina ndugu, ninawasihi kwa huruma za Mungu, mtoe miili yenu+ iwe dhabihu iliyo hai, takatifu,+ na yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri.+  Na acheni kufinyangwa na mfumo huu wa mambo,* bali mgeuzwe kwa kufanya upya akili yenu,+ ili mjihakikishie wenyewe+ mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.  Kwa maana kupitia fadhili zisizostahiliwa nilizopewa ninamwambia kila mtu kati yenu asijifikirie mwenyewe kuliko ilivyo lazima kufikiri,+ bali afikiri ili awe na akili timamu, kila mmoja kama Mungu alivyompa* kipimo cha imani.+  Kwa maana kama vile tulivyo na viungo vingi katika mwili mmoja,+ lakini viungo hivyo havifanyi kazi ileile,  ndivyo sisi, ingawa tuko wengi, ni mwili mmoja katika muungano na Kristo, lakini kila mmoja wetu ni kiungo cha mwingine.+  Basi, kwa kuwa tuna zawadi zinazotofautiana kulingana na fadhili zisizostahiliwa tulizopewa,+ kama ni ya unabii, na tutoe unabii kulingana na imani yetu;  au kama ni ya huduma, na tuwe katika huduma hii; au yule anayefundisha, na aendelee kufundisha;+  au yule anayetia moyo,* na atie moyo;*+ yule anayegawa,* na afanye hivyo kwa ukarimu;+ yule anayesimamia,* na afanye hivyo kwa bidii;*+ yule anayeonyesha rehema, na afanye hivyo kwa uchangamfu.+  Upendo wenu na uwe bila unafiki.+ Chukieni maovu;+ shikamaneni na mema. 10  Katika upendo wa kindugu iweni na upendo mwororo kwa mtu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima, iweni wa kwanza.*+ 11  Iweni wenye bidii,* msiwe wavivu.*+ Wakeni roho.+ Mtumikieni Yehova.*+ 12  Shangilieni katika tumaini. Vumilieni chini ya dhiki.+ Dumuni katika sala.+ 13  Shirikini pamoja na watakatifu kulingana na mahitaji yao.+ Iweni wakaribishaji wageni.*+ 14  Endeleeni kuwabariki wale wanaowatesa;+ muwe mkibariki msiwe mkilaani.+ 15  Shangilieni na wale wanaoshangilia; lieni na wale wanaolia. 16  Wafikirieni wengine kama mnavyojifikiria; msikazie akili zenu kwenye mambo makuu,* bali mwongozwe na mambo ya hali ya chini.+ Msiwe wenye hekima machoni penu wenyewe.+ 17  Msimlipe yeyote uovu kwa uovu.+ Zingatieni mambo yaliyo mema kulingana na maoni ya* watu wote. 18  Ikiwezekana, kwa kadiri inavyowategemea ninyi, fanyeni amani na watu wote.+ 19  Wapendwa, msijilipizie kisasi bali iachieni nafasi ghadhabu;*+ kwa maana imeandikwa: “Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.”*+ 20  Lakini, “ikiwa adui yako ana njaa, mlishe; ikiwa ana kiu, mpe kitu anywe; kwa maana kwa kufanya hivyo utakusanya makaa ya mawe yanayowaka juu ya kichwa chake.”*+ 21  Usiache ushindwe na uovu, bali endelea kuushinda uovu kwa wema.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “alivyomgawia.”
Au “juhudi.”
Au “anayeongoza.”
Au “anayechangia.”
Au “ahimize.”
Au “anayehimiza.”
Au “chukueni hatua ya kwanza.”
Au “jitihada.”
Au “msiwe wavivu katika kazi zenu.”
Au “iweni wakarimu.”
Au “msifikirie makuu.”
Au “machoni pa.”
Yaani, ghadhabu ya Mungu.
Yaani, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.