Zaburi 140:1-13

  • Yehova ni Mwokozi mwenye nguvu

    • Waovu ni kama nyoka (3)

    • Watu wakatili wataangamia (11)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 140  Niokoe, Ee Yehova, kutoka kwa watu waovu;Nilinde kutoka kwa watu wakatili,+   Wale wanaopanga njama za uovu mioyoni mwao+Na kuchochea vita mchana kutwa.   Wanaunoa ulimi wao kama wa nyoka;+Sumu ya nyoka vipiri iko nyuma ya midomo yao.+ (Sela)   Nilinde, Ee Yehova, kutoka mikononi mwa waovu;+Nilinde kutoka kwa watu wakatili,Wale wanaopanga njama ya kunitega miguu.   Wenye kiburi huuficha mtego ili uninase;Kwa kamba wanautandaza wavu kando ya njia.+ Wanatega mitego ya kuninasa.+ (Sela)   Ninamwambia Yehova: “Wewe ni Mungu wangu. Sikiliza, Ee Yehova, sihi zangu za kuomba msaada.”+   Ee Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu, Mwokozi wangu mwenye nguvu,Wewe hukinga kichwa changu katika siku ya vita.+   Ee Yehova, usitosheleze tamaa za waovu. Usiruhusu njama zao zifanikiwe, ili wasijikweze. (Sela)+   Vichwa vya wale wanaonizingiraNa vifunikwe na uovu unaosemwa na midomo yao.+ 10  Makaa ya mawe yanayowaka na yawanyeshee kama mvua.+ Na watupwe motoni,Ndani ya mashimo yenye kina,*+ wasiinuke tena kamwe. 11  Mchongezi na asipate makao duniani.*+ Uovu na uwafuatie watu wakatili na kuwaangamiza. 12  Ninajua kwamba Yehova atawatetea watu wa hali ya chiniNa kuwatendea haki maskini.+ 13  Hakika waadilifu watalishukuru jina lako;Wanyoofu watakaa mbele za uso wako.*+

Maelezo ya Chini

Au “Mashimo yenye umajimaji.”
Au “nchini.”
Au “katika uwepo wako.”