Matendo ya Mitume 20:1-38

  • Paulo akiwa Makedonia na Ugiriki (1-6)

  • Eutiko afufuliwa huko Troa (7-12)

  • Kutoka Troa kwenda Mileto (13-16)

  • Paulo akutana na wazee wa Efeso (17-38)

    • Kufundisha nyumba kwa nyumba (20)

    • “Kuna furaha zaidi katika kutoa” (35)

20  Baada ya ghasia kutulia, Paulo akatuma watu wawaite wanafunzi, akawatia moyo na kuwaaga, kisha akaanza safari yake ya kwenda Makedonia.  Baada ya kupitia maeneo hayo na kuwatia moyo kwa maneno mengi wale waliokuwa huko, akafika Ugiriki.  Akakaa huko miezi mitatu, lakini kwa sababu Wayahudi walikuwa wametunga hila dhidi yake+ alipokuwa karibu kusafiri kwenda Siria, akaamua kurudi kupitia Makedonia.  Alienda pamoja na Sopatro mwana wa Piro wa Beroya, Aristarko+ na Sekundo wa Wathesalonike, Gayo wa Derbe, Timotheo+ na, kutoka wilaya ya Asia, Tikiko+ na Trofimo.+  Wanaume hao wakatangulia na kutusubiri huko Troa;  lakini sisi tukaanza kusafiri baharini kutoka Filipi baada ya Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu,+ siku tano baadaye tukawafikia huko Troa, tukakaa huko siku saba.  Siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekusanyika ili kupata mlo, Paulo akaanza kuwahutubia, kwa sababu angeondoka kesho yake; naye akarefusha hotuba yake mpaka katikati ya usiku.  Basi kulikuwa na taa nyingi katika chumba cha juu tulimokuwa tumekusanyika.  Kijana aitwaye Eutiko alikuwa ameketi dirishani, naye akalala usingizi mzito Paulo alipokuwa akiongea, basi akalemewa na usingizi, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu, akaokotwa akiwa amekufa. 10  Lakini Paulo akashuka kutoka ghorofani, akajitupa juu yake akamkumbatia+ na kusema: “Acheni kupiga kelele, kwa maana yuko hai.”*+ 11  Kisha akapanda ghorofani, akaanzisha mlo* na kula chakula. Akaendelea kuzungumza kwa muda mrefu, mpaka mapambazuko, kisha akaondoka. 12  Basi wakamchukua mvulana huyo akiwa hai, wakafarijika sana. 13  Sasa tukaenda kwenye meli na kusafiri mpaka Aso, ambako tulikusudia kumchukua Paulo, kwa maana baada ya kutuagiza hivyo, alikusudia kwenda huko kwa miguu. 14  Basi alipotufikia huko Aso, akapanda kwenye meli tulimokuwa, tukaenda Mitilene. 15  Tukaondoka huko kesho yake, tukafika karibu na Kio, lakini siku ya pili tukafika Samo, na siku iliyofuata tukafika Mileto. 16  Paulo alikuwa ameamua kuendelea na safari bila kupitia Efeso,+ ili asitumie muda wowote katika mkoa wa Asia, kwa maana alikuwa akiharakisha kufika Yerusalemu+ siku ya Sherehe ya Pentekoste kama ingewezekana. 17  Hata hivyo, kutoka Mileto akatuma watu kwenda Efeso wawaite wazee wa kutaniko hilo waje. 18  Walipokuja akawaambia: “Mnajua vema jinsi nilivyotenda kati yenu tangu siku ya kwanza niliyokanyaga mkoa wa Asia,+ 19  nilivyomtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote*+ na machozi na majaribu yaliyonipata kupitia hila za Wayahudi, 20  nami sikuepuka kuwaambia ninyi jambo lolote lenye faida* na kuwafundisha hadharani+ na nyumba kwa nyumba.+ 21  Lakini nilitoa ushahidi kikamili kwa Wayahudi na Wagiriki kuhusu toba+ kwa Mungu na kuwa na imani katika Bwana wetu Yesu.+ 22  Na sasa, tazameni! nikiwa nimefungwa katika* roho, ninasafiri kwenda Yerusalemu, ingawa sijui mambo yatakayonipata huko, 23  isipokuwa kutoka jiji mpaka jiji roho takatifu inanitolea ushahidi tena na tena, ikisema kwamba nitafungwa gerezani na kupatwa na dhiki.+ 24  Hata hivyo, sioni uhai wangu* kuwa muhimu kwangu,* mradi tu nimalize mwendo wangu+ na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu. 25  “Na sasa, tazameni! ninajua kwamba hakuna yeyote kati yenu ninyi niliowahubiria kuhusu Ufalme atakayeona uso wangu tena. 26  Basi ninawaita ili mshuhudie leo hii kwamba mimi sina hatia ya damu ya mtu yeyote,+ 27  kwa maana sikukosa kuwaambia mashauri yote ya* Mungu.+ 28  Jiangalieni wenyewe+ na kundi lote, ambalo kati yake roho takatifu imewaweka ninyi rasmi muwe waangalizi,+ mlichunge kutaniko la Mungu,+ ambalo alilinunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe.+ 29  Ninajua kwamba nitakapoondoka mbwamwitu wenye kukandamiza wataingia miongoni mwenu+ nao hawatalitendea kundi kwa wororo, 30  na kutoka miongoni mwenu watu watasimama na kusema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.+ 31  “Kwa hiyo endeleeni kukesha, na kukumbuka kwamba kwa miaka mitatu,+ usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mmoja wenu kwa machozi. 32  Na sasa ninawakabidhi ninyi kwa Mungu na kwa neno la fadhili zake zisizostahiliwa, ambalo linaweza kuwajenga na kuwapa urithi kati ya wale wote waliotakaswa.+ 33  Sikutamani fedha, dhahabu, wala mavazi ya mtu yeyote.+ 34  Ninyi wenyewe mnajua kwamba nimefanya kazi kwa hii mikono yangu ili kupata mahitaji yangu+ na ya wale walio pamoja nami. 35  Nimewaonyesha ninyi katika mambo yote kwamba kwa kufanya kazi kwa bidii hivyo,+ ni lazima mwasaidie walio dhaifu, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, aliposema: ‘Kuna furaha zaidi katika kutoa+ kuliko ilivyo katika kupokea.’” 36  Baada ya kusema mambo haya, akapiga magoti pamoja nao wote na kusali. 37  Kwa kweli, wote wakalia sana, nao wakamkumbatia Paulo* na kumbusu kwa upendo,* 38  kwa maana waliumia sana aliposema kwamba hawangeuona uso wake tena.+ Kisha wakamsindikiza mpaka kwenye meli.

Maelezo ya Chini

Au “nafsi yake imo ndani yake.”
Tnn., “akaumega mkate.”
Au “unyenyekevu wa akili.”
Au “kwa faida yenu.”
Au “nimechochewa na.”
Au “nafsi yangu.”
Au “ukiwa na thamani yoyote kwangu.”
Au “kusudi lote la.”
Tnn., “wakamwangukia Paulo shingoni.”
Au “wororo.”